Shirika la TECHNOSERVE limetoa mafunzo kwa maafisa ugani wa
kata za wilaya ya Kyela,katika ukumbi wa KBC(kyela bussines center) ambapo
maafisa ugani wamefundishwa juu ya namna ya kuwa shauri wakulima wa zao la
kakao kurekebisha mashamba na uanzishaji wa mashamba mapya,uchaguzi wa mbegu
bora na ustawishaji shambani.
Naye mkuu wa mafunzo kutoka shirika la TECHNOSERVE ndugu AZIZI
MWILA amesema lengo la mafunzo hayo ni kuongeza uelewa kwa maafisa ugani juu ya
kilimo na biashara ya zao la kakao katika Wilaya ya Kyela.
Mariamu Jonas Mlacha afisa ugani kutoka kata ya Ipinda
ametoa shukrani kwa Shirika hilo kwa niaba ya washiriki wa mafunzo hayo. Na Upendo Mzumbwe
No comments:
Post a Comment