Wednesday 27 May 2015

Rais Kikwete aahidi kupambana na maslahi ya walimu kabla ya kumaliza kipindi chake.


Rais Dokta.Jakaya Kikwete amesema serikali yake ya awamu ya nne inaendelea kujitahidi kuhakikisha kuwa changamoto sugu zinazowakabili walimu zinapatiwa ufumbuzi na kuandaa mazingira bora ya kuiwezesha serikali ya awamu ya tano kukamilisha ufumbuzi wa changamoto zitakazobaki.
Dokta.Kikwete ametoa kauli hiyo ya matumaini kwa walimu  wakati akizungumza na walimu wawakilishi wa chama cha walimu nchini wanaokutana jijini arusha.
 
Awali katika risala yake kwa rais,katibu mkuu wa CWT Alhaj Yahya Msulwa aliziainisha changamoto wanazokabiliana nazo walimu kuwa ni pamoja na maslahi duni,mazingira duni ya kazi na sua la upandishwaji wa madaraja na marekebisho ya mishahara ambalo anasema kikwazo kubwa kimekuwa ni watendaji hususani katika halmashauri za wilaya.
 
Mheshimiwa magreth sita  ni mwenyekiti mstaafu wa CWT anasema ili kuboresha elimu nchini ipo haja idara ya ukaguzi ikabadilishwa na kupewa wakala ili kuongeza kasi ya utendaji huku waziri wa elimu dakta shukuru kawambwa akitoa pongezi kwa CWT kwa kusaidia katika uboreshaji wa elimu nchini.
 
Mkutano huo mkuu wa CWT unafanyika sambamba na uchaguzi mkuu wa viongozi wa chama hicho katika ngazi ya kuanzia rais na makamu wake ,katibu mkuu na naibu wake pamoja na wajumbe. 
 

No comments: