Monday 8 February 2016

Wajane Wawili Wauawa Kwa Kukatwa Mapanga Wakidaiwa Kusambaza Kipindupindu Mkoani Mbeya


Wajane wawili wa Kitongoji cha Bulinda wilayani Kyela wameuawa kwa mapanga wakidaiwa kusambaza ugonjwa wa kipindupindu baada ya kufiwa na waume zao katika eneo hilo.

Waliouawa ni Geneli Kapwela (65) na Rahabu Bungulu (70) waliokuwa wakiishi peke yao.

Kamanda wa Polisi  Mkoa wa Mbeya  Ahmed  Msangi  alisema  jana kuwa  wajane  hao  waliuawa  juzi  baada  ya  kipindupindu  kuhusishwa  na  imani za kishirikina.

Takwimu  za  mauaji toka polisi zinaonyesha  karibu watu wawili wanauawa  mkoani  Mbeya  kwa  imani  za  kishirikina

No comments: