Friday 7 October 2016

TAMASHA LA NGOMA ZA JADI LA DK TULIA LAFANA WILAYANI RUNGWE


Mbunge viti maalum Mkoa wa Mbeya, Dk Mary Mwanjelwa akizungumza katika tamasha huku akiwa na wabunge wengine wa Mkoa wa MbeyaMbunge wa Lupa, Victor Mwambalaswa akimvalisha shuka mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos MakallaNaibu Spika, Dk Tulia Ackson akisaidiana na Wabunge kumvalisha shuka la heshima ya Wanyakyusa Mkuu wa Mkoa wa MbeyaMkuu wa Mkoa wa Mbeya akiwa meza kuu pamoja na viongozi wengine wakifuatilia mashindano ya ngoma za asiliBaadhi ya wananchi waliojitokeza kushuhudia mashindano ya ngoma za jadiBalozi wa Kenya nchini Tanzania akitoa salam katika TamashaWabunge mbali mbali wakicheza na Naibu SpikaNaibu Spika akizungumza lengo la kuandaa mashindano ya ngoma za JadiMkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makalla akitoa hotuba ya ufunguzi wa Tamasha la ngoma za JadiNaibu Spika akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya.

WATANZANIA wametakiwa kutumia sanaa na utamaduni kwa ajili ya kutangaza amani na mshikamano ikiwa ni pamoja na kuenzi mila na desturi ambazo zilianza kupotea.

 

Wito huo ulitolewa  na Balozi wa Kenya nchini Tanzania Chirau Mwakwere alipokuwa akitoa salam katika Tamasha la Ngoma za jadi lililoandaliwa na Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Tulia Akson Mwansasu linalofanyika kwa siku mbili katika viwanja vya Tandale Tukuyu wilayani Rungwe Mkoa wa Mbeya.

 

Balozi alisema Utamaduni pia unaweza kutumika katika kujenga mahusiano mazuri baina ya nchi na nchi ikiwa ni pamoja na kukutanisha watu wa aina mbali mbali kwa pamoja.

 

Akifungua Tamasha hilo, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makalla alimpongeza Naibu Spika kwa ubunifu na kuanzisha wazo la kushindanisha ngoma za jadi za Mbeya jambo alilosema litasaidia kufufua utamaduni uliofifia.

 

Alisema kupitia utamaduni huo kutangaza mila na desturi za wazawa, kutangaza vivutio vya utalii, kuelimisha na kufundisha jamii, kutengeneza ajira kwa vijana pamoja na kuchochea uzalendo kwa Taifa pamoja na kukuza Uchumi.

 

Aliongeza kuwa zoezi hilo linapaswa kuwa endelevu kwa kufanywa Mkoa wote pamoja na Taifa kwa ujumla ili vizazi vilivyopo na vijavyo viweze kukumbushwa utamaduni wa makabila yao.

 

Kwa upande wake Naibu Spika, Dk. Tulia Ackson Mwansasu alisema mashindano hayo yalianzia kwenye ngazi ya kijiji katika Halmashauri za Kyela, Rungwe na Busokelo ambapo walipatikana washindi na kushindanahadi ngazi za Wilaya ambao wanashindana kumpata mshindi mmoja atakaye ziwakilisha Wilaya za Kyela na Rungwe kwenda mkoani Dodoma.

 

Alisema katika mashindano hayo jumla ya vikundi 35 ambavyo 16 vinatoka Rungwe na 19 Wilaya za Kyela vinashindana katika aina 9 za ngoma za Jadi za Kabila la Wanyakyusa.

 

Aidha katika Tamasha hilo ambalo litafanyika kwa sku mbili kati ya Oktoba 7 na 8, mwaka huu limehudhuriwa na Wabunge zaidi ya 12 akiwepo Naibu Waziri wa Elimu Mhandisi Stellah Manyanya ambapo pia linatarajiwa kufungwa na Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Nape Nauye.

No comments: