Sunday 11 December 2016

MADA YA UJASIRIAMALI: TATIZO MTAJI NDIYO ISHU:

Karibu Jumapili hii katika mada ya ujasiriamali. Lengo letu kubwa ni kupata ujuzi, elimu au maarifa mbalimbali kupitia ukurasa huu.

Mada ya leo inajikita zaidi kwa watu ambao wamekuwa wakilia kuwa wanashindwa kufanya jambo fulani kwa sababu ya kukosa mtaji.

Hivi ni kweli kwa elimu, ujinga, ufahamu wako, maeneo unayoishi, namna unavyoishi inakosa mtaji.

Kilio kikubwa cha Wanadamu wengi duniani ni kuhusu mtaji, mtu anaamini akiwa na mtaji haweI kukosa cha kufanya lakini katika uhalisi ni kweli kwamba mtaji ndiyo kila kitu.

Ni kweli lakini si kweli, mtaji ambao wengi wamekuwa wakidhania ni fedha pekee, ila wanasahau kuwa kuna mtaji rasilimali watu, wanasahau mtaji inaweza kuwa rasilimali aridhi, wanasahau kuwa mtaji mkubwa ni kuwa na WAZO la kitu unachotaka kukifanya.

Unaweza kuwa na mtaji lakini ukakosa cha kufanya au kama utafanya basi utafanikiwa nimagumashimagumashi kwa sababu tu huna elimu na hicho kitu, hukuwa na wazo hilo miaka miwili kabla.

Ndiyo maana utasikia kuna misemo kama kubaka fani, kwa mtindo wako wa kupata pesa na kurukia kufanya biashara fulani, huko ni sawa na kuibaka hiyo biashara.

Mtaji haujawahi kuwa tatizo bali tatizo ni wewe mwenyewe, ingawa wengi wanaamini mtaji ni pesa kwa sababu ndizi zinazotumika katika maisha ya kila siku. kama kweli mtaji ni MAWAZO kwa nini usiyatumie yakupe mtaji pesa.

Kama mtaji ni watu kwa nini usiwatumie watu hao kukupatia mtaji utakaougeuza kuwa pesa. Kama mtaji ni aridhi mbona huitumii kwa kuigeuza kuwa pesa.

Hili ni tatizo, mtaji ni kile ulichonacho, achana na mawazo ya kutaka kupata mtaji pesa wakati wa mawazo, aridhi na watu hujautumia.

Acha kukilaumu kuwan
TATIZO ni mtaji, hata kama ndiyo unataka nani akutafutie huo mtaji, unadhani nani yuko tayari kukupa wewe mtaji pesa wakati mwezi wa kwanza ada imekaribia. Mama mwenye nyumba anadai hela ya pango, bili ya maji na umeme vinamsubiri.

Umiza akili kutumia mtaji ulionao kuingiza pesa, leo hii kuna watu wanaishi kwa sababu tu walikuwa na wazo fulani ambalo waluligeuza nakuwa mtaji pesa.

Nimalize kwa kukaribisha ushauri au maoni ya moja kwa moja au inbox.

No comments: