Monday, 26 March 2018

KIMBIA MPENZI TUTAKUTANA MBELE KWA MBELE!! (Sehemu ya 10)


                                                    (the first run away love to told by Deogratius gift kipapa.)
EPISODI 10
INTRO:
Simulizi ya msichana wa shule aliyelazimika kumtorosha mpenzi wake mbali na baba yake pamoja na serikali mara baada ya kumpa ujauzito. Kamwe hakufikiri kwamba kumruhusu akimbie ni kuliruhusu penzi lake lipotelee mbali milele.  Simulizi hii, haitakuonyesha ni jinsi gani ilivyo kutengana na mpenzi wako pekee bali pia itakushangaza zaidi na uhusiano wa baba na mwana ambao kamwe hukuwahi kuuvutia picha, kuna machozi, na jasho, mbio na kuvuta pumzi, kama ulisoma simulizi yoyote ya mapenzi kutoka kwa gift kipapa na kuhakikishia ya kwamba haujasoma kitu. This is not just a heart to heart story but I run away love which no one could never ever found.
ILIPOISHIA EPISODI 9….
“mambo ona! ona, mama ameninunulia kuku!”
Aliongea mtoto huyo mara baada ya kuingia na kuketi na mama yake , mikono yake ilikuwa imelishikilia paja la kuku  alilokuwa ameanza kulitafuna toka huko nje.
“oh , mama mzuri , kuku na nini?”
Aliuliza .
“na chips.”
Aliongea mtoto huyo huku akitabasamu.
“oh safi sana , mwambie ahsante mama.”
“ahsante mama.’
Mtoto huyo aliongea huku akimuangalia mama yake usoni.
MWENDELEZO WAKE:

MALUME TV

https://youtu.be/Bn6oIgWmTkg

Thursday, 22 March 2018

KIMBIA MPENZI TUTAKUTANA MBELE KWA MBELE!!(Sehemu 9)


                                                    (the first run away love to told by Deogratius gift kipapa.)
EPISODI 09
INTRO:
Simulizi ya msichana wa shule aliyelazimika kumtorosha mpenzi wake mbali na baba yake pamoja na serikali mara baada ya kumpa ujauzito. Kamwe hakufikiri kwamba kumruhusu akimbie ni kuliruhusu penzi lake lipotelee mbali milele.  Simulizi hii, haitakuonyesha ni jinsi gani ilivyo kutengana na mpenzi wako pekee bali pia itakushangaza zaidi na uhusiano wa baba na mwana ambao kamwe hukuwahi kuuvutia picha, kuna machozi, na jasho, mbio na kuvuta pumzi, kama ulisoma simulizi yoyote ya mapenzi kutoka kwa gift kipapa na kuhakikishia ya kwamba haujasoma kitu. This is not just a heart to heart story but I run away love which no one could never ever found.
ILIPOISHIA EPISODI 8….
Miti ya kibanda hicho ilivutana vutana , huku udongo uliokuwa umeishika miti hiyo pamoja na kamba vikidondoka chini , na kilicho fuata hapo ulikuwa mti mmoja mmoja kudondoka na baadae mianzi ya iliyolishikilia paa la nyasi yote ilidondoka , na mzee fanuel alitoka nje ya kibanda hicho huku akiyatupa tupa majani yaliyokuwa yamemzunguka mwilini mwake na kuyasukuma sukuma kwa panga lake, aliichukua bara bara na safari hii alikuwa anaelekea njia panda ya lufilyo  na huko alikuwa ana uhakika wa kukata miguu ya mtu, shingo yake kiuno chake au chochote lakini alihitaji mvulana huyo afe siku hiyo tena afe huku akiishuhudia damu yake ikivuja hadi tone la mwisho.
MWENDELEZO WAKE:
Watu wote waliokuwa kwenye vibanda vya jirani walitoka nje kuangalia shoo hiyo , hawakupiga yowe wala vifijo bali kila mmoja alimshtua mwenzake kwa kukonyezana.
Tangu walipomuona Wakati akimkumbatia Pendo na kuongea nae kimahaba asubuhi ya jana kila mmoja alijua kwamba siku kama hii ingekuja kwake.
Japo hawakutegemea kumuona mzee fanuel akiwa amepagawa kiasi hicho , japo kila mmoja alijua uhusiano wa Wakati na mzee huyo ulikuwa mzuri mno, kila mtu alikuwa akimuonea wivu jinsi ambavyo alikuwa akimuungusha. Na wakati mwingine alikuwa akiongea nae na kutania na nae kama rafiki.
Na kwa mtu aliyemjua vema mzee fanuel ilikuwa kweli kusema wakati alikuwa rafiki yake , alikuwa ni aina ya mwanaume ambae alikuwa hajichanganyi sana na wenzake , yeye alikuwa ni mtu wa nyumbani na ofisini na ukizungumzia kuhusu marafiki wakati wote alikuwa akizunguka na mkewe pamoja na binti yake , walizunguka kila mahali pamoja , iwe kanisani, sokoni au popote, na hilo lilimfanya aonekane mwanaume anayeipenda familia yake kuliko mwanaume yoyote hapo.
Na jambo lililokuwa linashangaza zaidi wakati ndio mvulana pekee aliyekuwa anauwezo wa kuongea na pendo mbele yake , wavulana wengine wote walikuwa wanamuogopa mwanaume huyo kama vile wanaogopa kifo. Na pengine walipaswa kufanya hivyo , walimuona kila hasubuhi akifanya mazoezi huwanjani na wala hakuwa anacheza mpira au kukimbia kama ilivyo kwa kila mmoja , bali yeye alikuwa akicheza kungfu , karate na tai kondo.
Kwa kweli alipaswa kuwa askari jeshi tena yule anayetumwa kwenye misheni za mauaji ya kivita , lakini yeye alikuwa ni daktari tu , alikuwa anajali macho ya kila mmoja .
Na alikuwa akipata tuzo ya udktari bora kila mwaka.
“aahhhhh, aaahhh!”
Ilikuwa ni sauti yake huku panga lake likizipiga piga nguzo za miti ya mianzi zilizokuwa zimekishikilia kipanda hicho na nacho pia kiliishia kama vile kilivyoishia kile kibanda cha makazi ya wakati .
Yani kama kweli wakati bado angekuwa ndani ya mji huo basi, angekuwa hana makazi usiku wa siku hiyo.
***
Yalikuwa ni majira ya saa saba na robo ya  mchana, Basi lilifunga breki yalikuwa ni maeneo ya ililula, mji mdogo uliojengeka kando kando ya bara bara katika mkoa wa iringa ambapo mabasi mbali mbali huwa yanasimama kwa muda kwa ajili ya abiria kupata chakula.
Kila mmoja alishuka kwa ajili ya kuingia kwenye migahawa iliyokuwa kando kando ya bara bara hiyo.
Lakini wakati alibaki , alifungua mkoba wake na kutoa mfuko wa plastiki , ambao Pendo alimpatia.
Alipoanza kuufungua mfuko huo aliiona sura ya pendo kwenye macho yake na masikioni mwake aliisikia sauti yake.
“ chakula usikifungue sasa hivi , nataka mpaka ukiwa ndani ya basi , nataka ule ukiwa unakikumbuka kwamba ndio chakula chako cha mwisho kula kutoka kwangu.”
Sauti hii toka kwa pendo ndio iliyosikika masikioni mwa wakati kwa muda huo na kumfanya aanze kudondosha machozi tena, na pale alipokifungua chakula hicho ndio machozi yaliongezeka, zilikuwa ni chapati na maharage , pendo alikuwa anajua ni jinsi gani wakati alikuwa anakipenda chakula hicho, kwa dakika hiyo kila kitu kiliwa kama kilivyokuwa , yalikuwa maumivu ambayo aliamini kamwe hayatakuja kukoma katika maisha yake, kukaa mbali na pendo lilikuwa ni jambo ambalo alikuwa analiogopa kuliko hata kifo.
Na leo jambo hilo limemtokea  chaguo pekee alilonalo kwa wakati huo ni kukimbia, alijua baba yake pendo kamwe asingeweza kumuangalia kama vile alivyokuwa akimuangalia kwa wakati wote .
Alikumbuka vile alivyokuwa akimuamini , na hata katika msiba wa bibi yake alikumbuka kuuona mkono wake ukilishika bega lake kumfariji, aliahidi kumsaidia japo hakuweka wazi msaada wake utakuwa wa aina gani, japo sasa hivi anaweza kuwa mtu pekee anayemtaka afie mbali au hata kutiwa mbaroni na kuchakaa jera , kwa sababu ameharibu kila kitu walichokijenga katika uhusiano wao.
“lakini nitarudi kwa aajili yako, pendo , haijalishi baba yako atakuwa ananichukia kiasi gani , nitarudi kwa ajili yako nay a mtoto wetu , naahidi.”
Alijisemesha kimoyo moyo huku machozi yakiendelea kumbubujika , abiria zaidi waliingia ndani ya basi wakiwa na vyakula walivyonunua, alipomuona yule mwanamke mwenye mtoto akiingia , wakati alijifuta uso wake haraka , na kuanza kula , alijua huyo mtoto akimkuta analia lazima atakuja na yale maswali yake ya udadisi, najibu lolote ambalo angelijibu ni lazima lingemfanya adondoshe machozi zaidi na hiyo ingekuwa aibu kwake.
“mambo ona! ona, mama ameninunulia kuku!”
Aliongea mtoto huyo mara baada ya kuingia na kuketi na mama yake , mikono yake ilikuwa imelishikilia paja la kuku  alilokuwa ameanza kulitafuna toka huko nje.
“oh , mama mzuri , kuku na nini?”
Aliuliza .
“na chips.”
Aliongea mtoto huyo huku akitabasamu.
“oh safi sana , mwambie ahsante mama.”
“ahsante mama.’
Mtoto huyo aliongea huku akimuangalia mama yake usoni.
Itaendelea kesho, pia unaweza kusoma stori sehemu ya mbele ya stori hii zaidi ya episodi 50 zipo tayari, pia unaweza kujipatia vitabu vyetu vingine kwa bei ya nafuu, kuna ofa ya vitabu kwa whatsap na inbox fb, viwili sh 1700 vitatu sh 2400
vinne sh 3200 vitano sh 4000,kimoja sh 1000.
Stori zetu zingine ni hizi zifuatazo:
NOT YOU NOW book 1 – 24 , MTOTO WA MTAA BOOK 1 – 20, I WILL HUNT YOU DOWN 1&2, WHEN I  SAY I LOVE 1 – 9, KIMBIA MPENZI BOOK 1,2,3,4,5 NA 6.  YOU CAN’T MAKE ME A FOOL AGAIN, SISTAHILI KUFUNGWA, NAIPENDA TANZANIA.
BABA WA KAMBO book01,02,03,
CHANGUO NGUO book01,02,03
TEKETEKE TAMU BOOK 01,02
YES BOSS BOOK 1,2, ASMA KIDOTI book 1,2,3 MSICHANA NYUMBA YA PILI BOOK1,2, KOCHA WA TENESI BOOK1,2, PITISHA KWENYE  MPASUO, WEZELE,
TWAMTOA MWARI book 1,2,
MCHEPUKO WA MSHUA, KITAA FLANI, MSAGAJI,
TAXI BUBU,
MAMA WA KAMBO BOOK 1,2,
DEMU WA GEREJI, MZEE WA CHUMVINI,
NATAKA ZOTE,
NIPE UTAMU KAKA JAMBAZI,
zamu zamu, OPARESHENI MAPENZI BOOK 1,2 JIRANI NYAMA YA HAMU BOOOK 1,2,3,4,5,6,7 NJOO MAMA HAYUPO 1,2,3,4,5,6 NATAKA UNIFUATE KICHAKANI BOOK 1,2,3,4,5 AISHA CHA UTAMU BOOK 1,2,3,4,5 KIDOLE AKINITOSHI BOOK 1,2,3  BEKI TATU WA MTAA BOOK 1,2,3,4
THE AFRICAN SEX MASHINE BOOK 1,2,3,4,5 na 6 KARIBU KITAA TICHA BOOK 
1,2,3,4,5 , KWAYA MASTA BOOK 1 , 2, 3 na 4 WIFI NIPE UTAMU … KAKA HAYUPO BOOK 1,2&3,4,5,6,7,  SHUGA MUMY LA 
KITASHA BOOK 1,2,3. MUUZA MAZIWA BOOK 1- 16, TOTO LA KISHUA 1- 9, SI UNA MATE NIMEKUSIA BOOK 1 – 5, HALO HALO 1-9, JIMAMA MTAA WA PILI 1 -8,
Namba zinazotumika kwa ajili ya malipo ni mpesa 0757 414 436 , tigo pesa 0715 557 191 airtel money 0789117674
Namba zote zimesajiliwa kwa jina la Deogratius Lwasye.

Tuesday, 20 March 2018

KIMBIA MPENZI TUTAKUTANA MBELE KWA MBELE!!(Sehemu ya 8)


                                                    (the first run away love to told by Deogratius gift kipapa.)
EPISODI 08
INTRO:
Simulizi ya msichana wa shule aliyelazimika kumtorosha mpenzi wake mbali na baba yake pamoja na serikali mara baada ya kumpa ujauzito. Kamwe hakufikiri kwamba kumruhusu akimbie ni kuliruhusu penzi lake lipotelee mbali milele.  Simulizi hii, haitakuonyesha ni jinsi gani ilivyo kutengana na mpenzi wako pekee bali pia itakushangaza zaidi na uhusiano wa baba na mwana ambao kamwe hukuwahi kuuvutia picha, kuna machozi, na jasho, mbio na kuvuta pumzi, kama ulisoma simulizi yoyote ya mapenzi kutoka kwa gift kipapa na kuhakikishia ya kwamba haujasoma kitu. This is not just a heart to heart story but I run away love which no one could never ever found.
ILIPOISHIA EPISODI 7….
“mamaaa, maamama , gari linaondoka.”
Aliongea mtoto huyo mara baada ya gari hilo kuanza safari.
“tulia wewe.’
Aliongea mama yake kwa ukali.
Basi hilo lilikuwa limefikia geti la kutokea katika stendi hiyo.
Maana yake safari ya kuuaga mji wa mbeya ndio ilikuwa inaanza rasmi, kila kitu kilikuwa kigeni kwa wakati ndani ya nusu saa , zile nyumba na makazi ya watu aliyoendelea aliyokuwa anayaona wakati basi hilo lilipo kuwa ndani ya mji wa mbeya vyote vilipotea ,  alichokiona kwa muda  huo yalikuwa nyumba moja moja zilizojitenga  na hii miti iliyokuwa kando ya bara bara iliyokuwa inarudi nyuma kwa kasi pamoja na milima na mambonde ambavyo vyote vilikuwa vikimshangaza kupita kiasi.
***
“ni wakati ! ni wakati!”
Aliongea pendo kwa woga huku akilia , muonekano wa baba yake ulikuwa ukimtisha kupita kiasi .
“wakati ? , wakati ndio nani?”
Aliuliza mzee fanuel kwa mshangao, kusema kweli alimjua wakati fika lakini kichwani kwake hakuwa mtu anayeweza kumfikiria kwa namna yoyote ile.
“yule mchoma kitimoto kule njia panda ya shule.”
Aliongea pendo huku akizidi kutetemeka , alijua akisema hivyo atamfanya baba yake akasirike zaidi .
“hapana , hapana , hawezi kuwa yeye , huwezi kunidharirisha kiasi hiki mwanangu , mimi ni daktari , mwanangu huwezi kudanganyika kwa vipande vya nyama , haiwezekani.’
Aliongea mzee fanuel akiwa amepagawa kabisa .
“ni yeye baba najua ni meku..”
“nyamaza , nyamaza pendo , huwezi kuniambia ni yeye huwezi .”
Alifoka baba yake na safari hii uso wake ulikuwa umebadilika kabisa alikuwa mnyama , tena mnya ma aliye tayari kumuumiza yoyote kwa kumrarua rarua , hilo lilimfanya pendo azidi kutetemeka kwa hofu .
Hakuongea na yoyote bali kutoka hapo sebuleni kuelekea stoo.
“fanuel hapana! Huwezi kufanya kile unachokifikiria , fanuel tafadhari nisikilize mkeo.”
Aliongea mama yake pendo akijaribu kumzuia lakini hilo lilikuwa jambo lisilowezekana mikono yake tayari ilikuwa imeshalishika panga na alitoka katika stoo hiyo kwa hasira huku akimsukumia mkewe kule.
Kwa kweli alikuwa nje ya akili yake , alikuwa tayari kulitumia vyovyote panga hilo mwilini kwa Wakati , iwe kumcharanga charanga , au kumchinja shingo yake avuje damu mpaka kufa na pengine hapo roho yake itaweza kutulia.
“fanuel hapana , fanuel rudi baba yangu , unakwenda kuiingiza familia yako yote katika matatizo, fanuel mume wangu!”
Mke wake alililia akimsihi arudi , macho yake yalikuwa yamejaa machozi tupu , alimjua mumewe akiwa katika hali hiyo anaweza kufanya lolote .
Pendo alikuwa kimya pale chini akiendelea kulia kwa kuguna guna , pasipo kuhofia kile baba yake anachokwenda kufanya alijua kwamba hakuna anacho kwenda kukutana nacho huko anakoelekea zaidi ya chumba kitupu.
Alifika kwenye nyumba hiyo huku akiwa amejaa hasira tupu , aliangalia kulia mhali na kuvalangua kila kilichokuwemo humo , kitanda alikituopa kule na kukifanya kigawanyike kila muanzi upande wake kamba iliyokuwa imefungwa kuishikiza mianzi hiyo haikufaa tena mikeka ndio aliirusha hovyo mara huku mara kule huku akiirarua rarua kwa panga lake. Alijua kwamba hakuna mtu humo lakini alitaka muda wowote atakapo rejea humo ajue kwamba yuko kwenye matatizo , na pale alipoangalia ukutani ndio hasira zilipo mjaa mara mbili zaidi , kulikuwa na karatasi gumu aina ya manira lilikuwa limebandikwa kwenye ukuta wa chumba hicho likiwa limechorwa mchoro mkubwa wa moyo , huku maneno yaliyoandikwa
“P and W are forever.” Zilikuwa ni herufi za majina yao na maneno ya kingereza yalikuwa na maana kwamba upendo wao ni wa milele.
Mzee fanuel kwa kweli alizidi kupagawa kwa hasira , alikuwa analikumbuyka karatasi hilo vizuri , lilikuwa lake na alimpa pendo, siku moja alipokuja ofisini mwake na kumuomba karatasi kwa ajili ya kuchorea mchoro wa moyo , alisema ni mradi ambao mwalimu aliwaagiza kila mmoja achore moyo wa binadamu jinsi unavyofaya kazi pamoja na mishipa yote inayoingiza na kutoa damu katika moyo , ni kweli alichora moyo lakini huu ulikuwa moyo ule wa mapendo aina ya kopa lavu na haiukuwa mradi wa shuleni bali mradi wa mapenzi.
“aahhhh!  Aaahhh!”
Mzee alipiga kelele kwa hasira huku akiivuta karatasi hiyo na kuichana chana kwa mikono yake.
“Wakati  popote ulipo wewe ni mtu mfu!!”
Aliongea mzee fanuel kwa hasira huku akiupiga ukuta wa kibanda hicho uliosilibwa kwa udongo  juu ya miti iliyopangwa kwa mpangilio mzuri, kibanda chote kilikuwa kikitikisika  na ni kama vile alikuwa anakwenda kukidondosha chini kwa ngumi zake hizo nzito.
Hakuna aliyemzuia  na hasira zake zilizidi kupanda zaidi na zaidi , kama yoyote yule angemkuta hapo asingeweza kufikiria kwamba mwanaume huyo ni daktari bingwa wa upasuaji wa macho , kwa kweli kila kitu hapo alikifanya kama vile mtu ambae hakulionja darasa hata moja .
Miti ya kibanda hicho ilivutana vutana , huku udongo uliokuwa umeishika miti hiyo pamoja na kamba vikidondoka chini , na kilicho fuata hapo ulikuwa mti mmoja mmoja kudondoka na baadae mianzi ya iliyolishikilia paa la nyasi yote ilidondoka , na mzee fanuel alitoka nje ya kibanda hicho huku akiyatupa tupa majani yaliyokuwa yamemzunguka mwilini mwake na kuyasukuma sukuma kwa panga lake, aliichukua bara bara na safari hii alikuwa anaelekea njia panda ya lufilyo  na huko alikuwa ana uhakika wa kukata miguu ya mtu, shingo yake kiuno chake au chochote lakini alihitaji mvulana huyo afe siku hiyo tena afe huku akiishuhudia damu yake ikivuja hadi tone la mwisho.
Itaendelea kesho, pia unaweza kusoma stori sehemu ya mbele ya stori hii zaidi ya episodi 50 zipo tayari, pia unaweza kujipatia vitabu vyetu vingine kwa bei ya nafuu, kuna ofa ya vitabu kwa whatsap na inbox fb, viwili sh 1700 vitatu sh 2400
vinne sh 3200 vitano sh 4000,kimoja sh 1000.
Stori zetu zingine ni hizi zifuatazo:
NOT YOU NOW book 1 – 24 , MTOTO WA MTAA BOOK 1 – 20, I WILL HUNT YOU DOWN 1&2, WHEN I  SAY I LOVE 1 – 9, KIMBIA MPENZI BOOK 1,2,3,4,5 NA 6.  YOU CAN’T MAKE ME A FOOL AGAIN, SISTAHILI KUFUNGWA, NAIPENDA TANZANIA.
BABA WA KAMBO book01,
CHANGUO NGUO book01,02,03
TEKETEKE TAMU BOOK 01,02
YES BOSS BOOK 1,2, ASMA KIDOTI book 1,2,3 MSICHANA NYUMBA YA PILI BOOK1,2, KOCHA WA TENESI BOOK1,2, PITISHA KWENYE  MPASUO, WEZELE,
TWAMTOA MWARI book 1,2,
MCHEPUKO WA MSHUA, KITAA FLANI, MSAGAJI,
TAXI BUBU,
MAMA WA KAMBO BOOK 1,2,
DEMU WA GEREJI, MZEE WA CHUMVINI,
NATAKA ZOTE,
NIPE UTAMU KAKA JAMBAZI,
zamu zamu, OPARESHENI MAPENZI BOOK 1,2 JIRANI NYAMA YA HAMU BOOOK 1,2,3,4,5,6,7 NJOO MAMA HAYUPO 1,2,3,4,5,6 NATAKA UNIFUATE KICHAKANI BOOK 1,2,3,4,5 AISHA CHA UTAMU BOOK 1,2,3,4,5 KIDOLE AKINITOSHI BOOK 1,2,3  BEKI TATU WA MTAA BOOK 1,2,3,4
THE AFRICAN SEX MASHINE BOOK 1,2,3,4,5 na 6 KARIBU KITAA TICHA BOOK 
1,2,3,4,5 , KWAYA MASTA BOOK 1 , 2, 3 na 4 WIFI NIPE UTAMU … KAKA HAYUPO BOOK 1,2&3,4,5,6,7,  SHUGA MUMY LA 
KITASHA BOOK 1,2,3. MUUZA MAZIWA BOOK 1- 16, TOTO LA KISHUA 1- 9, SI UNA MATE NIMEKUSIA BOOK 1 – 5, HALO HALO 1-9, JIMAMA MTAA WA PILI 1 -8,
Namba zinazotumika kwa ajili ya malipo ni mpesa 0757 414 436 , tigo pesa 0715 557 191 airtel money 0789117674
Namba zote zimesajiliwa kwa jina la Deogratius Lwasye.

Saturday, 17 March 2018

KIMBIA MPENZI TUTAKUTANA MBELE KWA MBELE!!(Sehemu ya 7)


                                                    (the first run away love to told by Deogratius gift kipapa.)
EPISODI 07
INTRO:
Simulizi ya msichana wa shule aliyelazimika kumtorosha mpenzi wake mbali na baba yake pamoja na serikali mara baada ya kumpa ujauzito. Kamwe hakufikiri kwamba kumruhusu akimbie ni kuliruhusu penzi lake lipotelee mbali milele.  Simulizi hii, haitakuonyesha ni jinsi gani ilivyo kutengana na mpenzi wako pekee bali pia itakushangaza zaidi na uhusiano wa baba na mwana ambao kamwe hukuwahi kuuvutia picha, kuna machozi, na jasho, mbio na kuvuta pumzi, kama ulisoma simulizi yoyote ya mapenzi kutoka kwa gift kipapa na kuhakikishia ya kwamba haujasoma kitu. This is not just a heart to heart story but I run away love which no one could never ever found.
ILIPOISHIA EPISODI 6….
“ndio lala mwanangu.”
Alimjibu mama yake.
“sawa kitanda kiko wapi?”
Aliuliza.
“lala hivyo hivyo bwana mi nimechoka .”
Aliongea mama huyo kwa ukali , sauti hiyo ilimtisha mwanae na kumfanya aanze kulia , kichwani mwake alifikiri mama yake atampiga muda huo huo.
“basi baba basi , nyamaza mwanangu.”
Aliongea mama huyo huku akimbembeleza mwanae mpaka akatulia. Wakati aliwaangalia kisha akaamuakugeukia upande wa dirishani , ambapo alijikuta amechukuliwa na usingi8zi dakika chache tu baada ya kufumba macho.
***
MWENDELEZO WAKE:
Alipofika mbeya mjini ilimbidi kulala ndani ya basi ili kuisubiri safari itakayofanyika alfajiri ya siku inayofuta basi hilo lililoandikwa KILIMANJARO ubavuni mwake lilikuwa na watu wengine wasiopungua ishirini ambao nao pia walitarajia kufanya safari aflajiri hiyo.
E11 ndio kiti ambacho wakati alikuwa amekalia, kililikuwa ni kiti cha dirishani , alichagua kiti hicho ili awe anaona mazingira basi likiwa safarini.
“mama, mama ,mbona basi aliendi?”
Aliomngea mtoto mmoja aliyekuwa amekaa na mma yake kicha pembeni ya wakati .
“litaenda tu mwanangu subiri kwanza tukiamka.”
Aliongea mama wa mtoto huyo.
“nilale?”
Aliuliza mtoto huyo.
“ndio lala mwanangu.”
Alimjibu mama yake.
“sawa kitanda kiko wapi?”
Aliuliza.
“lala hivyo hivyo bwana mi nimechoka .”
Aliongea mama huyo kwa ukali , sauti hiyo ilimtisha mwanae na kumfanya aanze kulia , kichwani mwake alifikiri mama yake atampiga muda huo huo.
“basi baba basi , nyamaza mwanangu.”
Aliongea mama huyo huku akimbembeleza mwanae mpaka akatulia. Wakati aliwaangalia kisha akaamuakugeukia upande wa dirishani , ambapo alijikuta amechukuliwa na usingi8zi dakika chache tu baada ya kufumba macho.
***
Unamtetea unajua alichokifanya.”
Aliongea mama yake pendo kwa ukali huku akihema mara baada ya mr.fanuel kumvuta pendo kutoka mikononi mwake.
“hata kama angefanya nini huwezi kumpiga mwanangu kiasi hiki, mtoto mwenyewe mmoja alafu unataka umuweke mialama alama.”
Aliongea mr. fanuel kwa ukali.
“unaenda wapi chukua barua yako huku.”
Aliongea mama yake pendo , huku akimshika shati alipotaka kuondoka na pendo.
“niache nikambembeleze mwanangu huko.”
Aliongea kwa ukali na kupokonyoa shati lake kwenye mikono ya mkewe.
“nyamaza mwanangu.”
Aliongea mr.fanuel huku akimpiga piga pendo mgongoni.
“kwa taarifa yako ana mimba huyo.”
Aliongea mama yake pendo, kauli iliyoingia moja kwa moja kwenye moyo wa mr.fanuel , aliacha kufanya kile alichokuwa anafanya na kisha ukimya ukatanda ghafla kati yao, hata zile kwikwi zilizokuwa zikisikika pendo alipokuwa analia zilikatika ghafla.
Pale mr.fanuel alipogeuka kumuangalia pendo usoni macho yao hayakugongana tena, pendo hakuweza kunyanyua kichwa chake lakini hili kofi zito kutoka kwa baba yake lilibadilisha kila kitu, alipepesuka na kudondoka chini huku akiwa haamini kwamba kofi zito kama hilo lilitoka kwa baba yake , alijaribu kumuangalia usoni na kwa kufanya hivyo ndio alijikuta anaogopa zaidi , hakukutana na lile tabasamu alilozoea kukutana nalo kila siku, huu uso haukuwa uso wa baba yake , labda mwingine mwili mzima wa pendo ulikuwa ukitetemeka ni kama vile anakwenda kufa.
“ni nani aliyefanya haya?”
Aliuliza mr. fanuel kwa sauti nzito iliyomtetemesha pendo kupita kiasi , alitamani ardhi ipasuke ili atumbukie kwenye bonde la  ufa litakalojitokeza na kupotelea huko.
Honi  za magari zilisikika na kumfanya kwa fujo na kumfanya Wakati azinduke toka kwenye usingizi mzito uliokuwa umemchukua.
“kumekucha!”
Aliongea kwa mshangao mara baada ya kuona mwanga uliokuwa umetanda angani huku pirika pirika za watu katika stendi hiyo zikiwa zimesha anza.
Ilikuwa aibu yeye peke yake ndio alikuwa amelala hadi wakati huo, kila mtu alikuwa macho na basi lilikuwa limekwishajaa .
Injini ilikuwa imewashwa na dereva alikuwa tayari kuliondosha basi hilo muda wowote.
“mamaaa, maamama , gari linaondoka.”
Aliongea mtoto huyo mara baada ya gari hilo kuanza safari.
“tulia wewe.’
Aliongea mama yake kwa ukali.
Basi hilo lilikuwa limefikia geti la kutokea katika stendi hiyo.
Maana yake safari ya kuuaga mji wa mbeya ndio ilikuwa inaanza rasmi, kila kitu kilikuwa kigeni kwa wakati ndani ya nusu saa , zile nyumba na makazi ya watu aliyoendelea aliyokuwa anayaona wakati basi hilo lilipo kuwa ndani ya mji wa mbeya vyote vilipotea ,  alichokiona kwa muda  huo yalikuwa nyumba moja moja zilizojitenga  na hii miti iliyokuwa kando ya bara bara iliyokuwa inarudi nyuma kwa kasi pamoja na milima na mambonde ambavyo vyote vilikuwa vikimshangaza kupita kiasi.
***
Itaendelea kesho, pia unaweza kusoma stori sehemu ya mbele ya stori hii zaidi ya episodi 50 zipo tayari, pia unaweza kujipatia vitabu vyetu vingine kwa bei ya nafuu, kuna ofa ya vitabu kwa whatsap na inbox fb, viwili sh 1700 vitatu sh 2400
vinne sh 3200 vitano sh 4000,kimoja sh 1000.
Stori zetu zingine ni hizi zifuatazo:
NOT YOU NOW book 1 – 24 , MTOTO WA MTAA BOOK 1 – 20, I WILL HUNT YOU DOWN 1&2, WHEN I  SAY I LOVE 1 – 9, KIMBIA MPENZI BOOK 1,2,3,4,5 NA 6.  YOU CAN’T MAKE ME A FOOL AGAIN, SISTAHILI KUFUNGWA, NAIPENDA TANZANIA.
BABA WA KAMBO book01,
CHANGUO NGUO book01,02,03
TEKETEKE TAMU BOOK 01,02
YES BOSS BOOK 1,2, ASMA KIDOTI book 1,2,3 MSICHANA NYUMBA YA PILI BOOK1,2, KOCHA WA TENESI BOOK1,2, PITISHA KWENYE  MPASUO, WEZELE,
TWAMTOA MWARI book 1,2,
MCHEPUKO WA MSHUA, KITAA FLANI, MSAGAJI,
TAXI BUBU,
MAMA WA KAMBO BOOK 1,2,
DEMU WA GEREJI, MZEE WA CHUMVINI,
NATAKA ZOTE,
NIPE UTAMU KAKA JAMBAZI,
zamu zamu, OPARESHENI MAPENZI BOOK 1,2 JIRANI NYAMA YA HAMU BOOOK 1,2,3,4,5,6,7 NJOO MAMA HAYUPO 1,2,3,4,5,6 NATAKA UNIFUATE KICHAKANI BOOK 1,2,3,4,5 AISHA CHA UTAMU BOOK 1,2,3,4,5 KIDOLE AKINITOSHI BOOK 1,2,3  BEKI TATU WA MTAA BOOK 1,2,3,4
THE AFRICAN SEX MASHINE BOOK 1,2,3,4,5 na 6 KARIBU KITAA TICHA BOOK 
1,2,3,4,5 , KWAYA MASTA BOOK 1 , 2, 3 na 4 WIFI NIPE UTAMU … KAKA HAYUPO BOOK 1,2&3,4,5,6,7 , SHUGA MUMY LA 
KISTASHA BOOK 1,2,3. MUUZA MAZIWA BOOK 1- 16 , TOTO LA KISHUA 1- 9 , SI UNA MATE NIMEKUSIA BOOK 1 – 5,HALO HALO 1-9 JIMAMA MTAA WA PILI 1 -8
Namba zinazotumika kwa ajili ya malipo ni mpesa 0757 414 436 , tigo pesa 0715 557 191 airtel money 0789117674
Namba zote zimesajiliwa kwa jina la Deogratius Lwasye

Thursday, 15 March 2018

KIMBIA MPENZI TUTAKUTANA MBELE KWA MBELE!!(Sehemu ya 6)


                                                    (the first run away love to told by Deogratius gift kipapa.)
EPISODI 06
INTRO:
Simulizi ya msichana wa shule aliyelazimika kumtorosha mpenzi wake mbali na baba yake pamoja na serikali mara baada ya kumpa ujauzito. Kamwe hakufikiri kwamba kumruhusu akimbie ni kuliruhusu penzi lake lipotelee mbali milele.  Simulizi hii, haitakuonyesha ni jinsi gani ilivyo kutengana na mpenzi wako pekee bali pia itakushangaza zaidi na uhusiano wa baba na mwana ambao kamwe hukuwahi kuuvutia picha, kuna machozi, na jasho, mbio na kuvuta pumzi, kama ulisoma simulizi yoyote ya mapenzi kutoka kwa gift kipapa na kuhakikishia ya kwamba haujasoma kitu. This is not just a heart to heart story but I run away love which no one could never ever found.
ILIPOISHIA EPISODI 5….
“nitakusubiri mpenzi wangu, mimi na mwanetu tutakusubiri , najua utarejea, ninakwamini.”
Aliongea pendo kwa kupaza sauti.
“usijali mpenzi wangu , nakupenda sana , nakuahidi nitarejea.”
Wakati nae pia alipaza sauti , macho yao yalikuwa yakiangaliana , basi hilo lilitimua mbio na kuchanganya vumbi lililoipoteza picha  iliyokuwa kati yao , hakuna aliyekuwa anamuona mwenzake tena , bali vumbi zito lililomfanya kila mmoja akohoe na kuyafumba macho yake na hivyo ndivyo ilivyokuwa maono ya kila mmoja yalifunikwa na vumbi hilo na hivyo ndivyo walivyoagana, pendo alibaki amesimama akilia , huku wakati nae pia ndani ya basi akilia.
watu waliokuwa wakiwaangalia na waliwaona wa ajabu kweli.
MWENDELEZO WAKE:
E6
Alishindwa kabisa kujizuia, kutengana na Wakati lilikuwa pigo kubwa sana kwake,  machozi yaliendelea kumbubujika hata mbele ya mama yake , na kumganya mama yake ashtuke.
“pendo , unanini wewe?”
Aliuliza mama yake huku akishangaa.
Pendo alishindwa kumjibu lolote zaidi ya kumkabidhi barua aliyopewa shuleni.
“ya nini ?”
Aliuliza mama yake huku akiipokea , alianza kuifungua barua hiyo huku akimungalia pendo usoni, bado alikuwa analia.
“eti?”
Aliuliza mama yake kwa mshtuko mara baada ya kuifungua barua hiyo na kusoma haraka ili kupata kiini .
“Mungu wangu, we mtoto ni balaa gani hili ulilonitafutia!”
Aliuliza mama yake kwa mshituko huku pendio akiendeleza kilio cha kwikwi.
‘nani aliyekufanya hivi mwanangu?”
Aliuliza mama yake , na pendo aliendelea kulia tu bila kujibu lolote , jambo lililomfanya mama yake apatwe na hasira na kujikuta anamzaba kipao cha uso.
Hapo sasa kilio cha pendo kiliongezeka maumivu yote aliyokuwa anayapata moyoni sababu ya kutengana na mpenzi wake ndio kama vile yalifunguliwa na kibao hicho.
Mama yake alizidi kukasirika na kujikuta anampiga kibao kingine na kingine, pendo alizidi kulia kama vile mwenda wazimu.
“mwache , mwache mtoto , muache nimesema.”
Ilizikika sauti hiyo kwa ukali , alikuwa ni mzee Fanuel, baba yake pendo.
Mkoba wake aliuachia ukadondoka chini kisha haraka akaenda kumvuta binti yake toka kwa mkewe na kumkumbatia.
“nyamaza , nyamaza mama.”
Aliongea mr.fanuel huku akimbembeleza mwanae.
***
Alipofika mbeya mjini ilimbidi kulala ndani ya basi ili kuisubiri safari itakayofanyika alfajiri ya siku inayofuta basi hilo lililoandikwa KILIMANJARO ubavuni mwake lilikuwa na watu wengine wasiopungua ishirini ambao nao pia walitarajia kufanya safari aflajiri hiyo.
E11 ndio kiti ambacho wakati alikuwa amekalia, kililikuwa ni kiti cha dirishani , alichagua kiti hicho ili awe anaona mazingira basi likiwa safarini.
“mama, mama ,mbona basi aliendi?”
Aliomngea mtoto mmoja aliyekuwa amekaa na mma yake kicha pembeni ya wakati .
“litaenda tu mwanangu subiri kwanza tukiamka.”
Aliongea mama wa mtoto huyo.
“nilale?”
Aliuliza mtoto huyo.
“ndio lala mwanangu.”
Alimjibu mama yake.
“sawa kitanda kiko wapi?”
Aliuliza.
“lala hivyo hivyo bwana mi nimechoka .”
Aliongea mama huyo kwa ukali , sauti hiyo ilimtisha mwanae na kumfanya aanze kulia , kichwani mwake alifikiri mama yake atampiga muda huo huo.
“basi baba basi , nyamaza mwanangu.”
Aliongea mama huyo huku akimbembeleza mwanae mpaka akatulia. Wakati aliwaangalia kisha akaamuakugeukia upande wa dirishani , ambapo alijikuta amechukuliwa na usingi8zi dakika chache tu baada ya kufumba macho.
***
Itaendelea kesho, pia unaweza kusoma stori sehemu ya mbele ya stori hii zaidi ya episodi 50 zipo tayari, pia unaweza kujipatia vitabu vyetu vingine kwa bei ya nafuu, kuna ofa ya vitabu kwa whatsap na inbox fb, viwili sh 1700 vitatu sh 2400
vinne sh 3200 vitano sh 4000,kimoja sh 1000.
Stori zetu zingine ni hizi zifuatazo:
NOT YOU NOW book 1 – 24 , MTOTO WA MTAA BOOK 1 – 20, I WILL HUNT YOU DOWN 1&2, WHEN I  SAY I LOVE 1 – 9, KIMBIA MPENZI BOOK 1,2,3,4,5 NA 6.  YOU CAN’T MAKE ME A FOOL AGAIN, SISTAHILI KUFUNGWA, NAIPENDA TANZANIA.
BABA WA KAMBO book01,
CHANGUO NGUO book01,02,03
TEKETEKE TAMU BOOK 01,02
YES BOSS BOOK 1,2, ASMA KIDOTI book 1,2,3 MSICHANA NYUMBA YA PILI BOOK1,2, KOCHA WA TENESI BOOK1,2, PITISHA KWENYE  MPASUO, WEZELE,
TWAMTOA MWARI book 1,2,
MCHEPUKO WA MSHUA, KITAA FLANI, MSAGAJI,
TAXI BUBU,
MAMA WA KAMBO BOOK 1,2,
DEMU WA GEREJI, MZEE WA CHUMVINI,
NATAKA ZOTE,
NIPE UTAMU KAKA JAMBAZI,
zamu zamu, OPARESHENI MAPENZI BOOK 1,2 JIRANI NYAMA YA HAMU BOOOK 1,2,3,4,5,6,7 NJOO MAMA HAYUPO 1,2,3,4,5,6 NATAKA UNIFUATE KICHAKANI BOOK 1,2,3,4,5 AISHA CHA UTAMU BOOK 1,2,3,4,5 KIDOLE AKINITOSHI BOOK 1,2,3  BEKI TATU WA MTAA BOOK 1,2,3,4
THE AFRICAN SEX MASHINE BOOK 1,2,3,4,5 na 6 KARIBU KITAA TICHA BOOK 
1,2,3,4,5 , KWAYA MASTA BOOK 1 , 2, 3 na 4 WIFI NIPE UTAMU … KAKA HAYUPO BOOK 1,2&3,4,5,6,7 , SHUGA MUMY LA 
KISTASHA BOOK 1,2,3. MUUZA MAZIWA BOOK 1- 16 , TOTO LA KISHUA 1- 9 , SI UNA MATE NIMEKUSIA BOOK 1 – 5,HALO HALO 1-9 JIMAMA MTAA WA PILI 1 -8
Namba zinazotumika kwa ajili ya malipo ni mpesa 0757 414 436 , tigo pesa 0715 557 191 airtel money 0789117674
Namba zote zimesajiliwa kwa jina la Deogratius Lwasye

Wednesday, 14 March 2018

wanajeshi Anayedaiwa kuua askari mwenzake apandishwa kizimbani


Mwanajeshi MT 109795 Private Ramadhan Mlaku (28) amefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akikabiliwa na shitaka la mauaji ya askari mwenzie, MT 79512 SGT Saimon Munyama.
Mshtakiwa huyo alifikishwa mahakamani hapo leo Jumatano Machi 14, 2018 saa tano asubuhi na gari la kubebea wagonjwa.
Alishushwa katika gari hilo akiwa juu ya kitanda cha wagonjwa na kupelekwa chumba cha mawakili wa Serikali ambapo alisomewa shtaka linalomkabili.
Akisomewa shtaka mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba wakili wa Serikali, Mosii Kaima amesema mtuhumiwa huyo anadaiwa kufanya kosa hilo Oktoba 30, 2017.
Imedai kuwa mshtakiwa ambaye ni mwanajeshi wa kambi ya Jeshi Makongo siku hiyo akiwa Makao Mkuu ya JWTZ Upanga, Dar es Salaam alimuua askari mwenzie MT 79512 SGT Munyama.
Baada ya kusomewa shtaka hilo, mshtakiwa huyo hakuruhusiwa kuongea chochote kwa sababu Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu haina mamlaka ya kuisikiliza kesi hiyo.
Pia kosa hilo hakuna dhamana kwa mujibu wa sheria.
Upande wa mashtaka ulidai kuwa upelelezi bado haujakamilika na Hakimu Simba aliutaka upande wa mashtaka kujitahidi kukamilisha upelelezi wa kesi hiyo mapema.
Kesi imeahirishwa hadi Machi 28, 2018 kwa ajili ya kutajwa ili kuangalia kama upelelezi utakuwa umekamilika ama la.
Baada ya kusomewa shtaka hilo mshtakiwa huyo alipandishwa tena katika gari la wagonjwa na kurudishwa mahabusu.