Monday, 1 June 2015

Wanachama wa CCM Igunga kufunga ofisi ya katibu wa chama hicho na kutaka ang"olewe kwa matumizi mabaya ya madaraka.


Baadhi ya wanachama wa chama cha mapinduzi wilaya ya igunga wametishia kufunga ofisi ya chama kushinikiza katibu wa CCM wilaya hiyo aondolewe kwa madai ya matumizi mabaya ya madaraka ikiwemo kufuja fedhazinazotolewa na wadau kwa ajili ya kusaidia vijana hatua ambayo imesababisha mgawanyiko mkubwa kwa wanachama hususani wakati huu mgumu  wa kuelekea  katika mchakato wa uchaguzi mkuu.

Mapema asubuhi baadhi ya wanachama wazee na vijana wameonekana wakiwa jazba ya kutaka kufunga ofisi huku wameshika mabango yenye ujumbe mbalimbali wa kutaka uongozi wa juu kumuondoa katibu wa chama cha mapinduzi wilaya ya igunga bw.abdallah kazwika,wakimtuhumu kutumia vibaya madaraka yake.
 
Kufuatia hali hiyo mkuu wa wilaya ya igunga Bi.Zipora Pangani alifika katika ofisi za ccm ambapo kabla ya kusikiliza hoja na madai ya wanachama hao alitoa amri kali ya kuwataka waondoke maeneo ya ofisi yao hatua ambayo ilipingwa na wanachama hao huku walalamikia hatua ya mkuu huyo wa wilaya kwamba ameingilia uhuru wa wanachama kwa kutumia nguvu ya madaraka aliyopewa na serikali.
 
Hata hivyo jeshi la Polisi wilayani igunga lilitumia busara pasipo  kutumia nguvu kama ilivyozoeleka katika matukio mengine kuwatawanya  wanachama hao huku katibu  wa  ccm wilaya ya igunga Bw.Abdallah  Kazwika akipinga tuhuma hizo dhidi yake.
 

No comments: