Mgogoro
wa ardhi kugombea mpaka kati ya kijiji cha Olkung'wadu wilaya ya
Arumeru na Lekimurunyi wilaya ya sia umeingia katika hatua ya uvunjifu
wa amani baada ya watu wanaodaiwa kutoka kijiji cha Lekimurunyi wakiwa
na silaa za jadi kuvamia kijiji cha Olkung’wado kufeka zaidi ya hekari
thelasini za mzao ya mahindi na nyanya pamoja na kubomoa vibanda wanavyo
ishi kwa muda wakiwa shambani.
Wakizungumza na ITV iliyofika katika eneo ilo na kushuhudia
uharibifu uliyofanyika wakazi wa kijiji cha Olkugw’ado waliyo patwa na
mkasa huo wamesema tukio ilo limefanywa usiku na kundi la watu waliyo
ingia katika mashamba kuwakimbiza wakulima na kisha kufeka na kuharibu
mazao hayo ambayo tayari yalikuwa yamekomaa.
Mwenyekiti wa kitongoji cha Orok mahali palipo fanyika uharibifu
Terewali Nko amesema wakazi wa eneo ilo wanaishi kwa mashaka makubwa
kutokana na tishio la uvamizi wa kutumia silaa unatokea mara kwa mara na
ameiomba serikali ichukue hatua.
Kwa upande wake mbunge wa Arumeru mashariki Joshua Nasari amesema
anashindwa kuelewa kwanini serikali mbili za mkoa wa Kilimanjaro na
Arusha zinashindwa kumaliza mgogoro huo wa muda mrefu na kwamba kuna
kila dalili za kutokea kwa umwagaji wa damu kutoka na hali inavyo
endelea lakini yeye anaendelea na juhudi za kumaliza mgogoro huo.
No comments:
Post a Comment