SIKU chache baada ya wakazi wa Jiji la Mbeya kupewa tahadhari  juu
 ya uwepo wa nyoka mkubwa aina ya Chatu katika maeneo ya Rift Valley 
pembezoni mwa mto Meta uliopo jijini hapa juhudi za kumsaka zaanza kuzaa
 matunda.
 Juhudi
 za kumsaka Chatu huyo zilianza juzi kwa ushirikiano wa Wataalamu wa 
Wanyamapori pamoja na waganga wa jadi ambao walikuwa wakimsaka pembezoni
 mwa mtu huo.
 Hata
 hivyo jitihada za klumsaka Nyoka huyo zilianza kuzaa matunda baada ya 
jana asubuhi Waganga hao kufanikiwa kumnasa Chatu mdogo pembezoni mwa 
Mto Meta karibu na Hoteli ya Rift Valley.
 Kwa
 mujibu wa Mganga huyo, Mazoea Hamis(39) mkazi wa Chalinze mkoani Pwani 
alisema siku ya kwanza ya zoezi hilo walifanikiwa kugundua njia 
alimokuwa amepita lakini hawakufanikiwa kumpata.
 Alisema
 jioni yake baada ya kupumzika waliona waweke dawa za kienyeji ambazo 
zingiweza kumtoa mafichoni na kusogea karibu ambapo asubuhi waliwahi 
kuendelea kumtafuta.
Alisema
 baada ya muda kidogo wakati akiendelea kufyeka vichaka lakini kwa 
bahati nzuri alimkanyaga chatu huyo na yeye kukurupuka ndipo 
alipofanikiwa kumkamata.
Kwa
 mujibu wa mganga huyo ambaye anasaidiwa na Athman Keneth(30) mkazi wa 
Chunya mkoani hapa, alisema Chatu huyo ni mdogo na juhudi za kuendelea 
kumtafuta mkubwa zitaendelea kama kweli yupo.
Alisema
 mara nyingi Chatu mdogo anapoonekana Mkubwa anakuwa amehama ili 
kuwapisha wadogo kuendelea na maisha yao ama huyo mdogo alisombwa na 
maji kipindi cha mvua kutoka kwenye hifadhi na wenzie.
Hata
 hivyo taarifa kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Jiji zinadai kuwa baada ya 
kukamatwa kwa Chatu huyo atahifadhiwa na kutunzwa katika Hifadhi ya 
Wanyama ya Ifisi ambako kuna wanyamapori wengine wa maonesho.
NA MBEYA YETU 





No comments:
Post a Comment