Tuesday 29 May 2018

Mfaransa Simba ataka Mil 90 kwa mwezi

Kocha wa Simba, Mfaransa Pierre Lechantre kwa sasa analipwa mshahara wa Sh.45 milioni kwa mwezi na Mtunisia, Aymen Habib Mohammed anachukua Sh 23 milioni kwa mwezi lakini kama Simba itabadili mawazo na kumpa mkataba mpya sharti lake la kwanza ni mshahara kupandishwa kwa asilimia 100.
Hiyo inamaanisha kwamba kama viongozi wakikubaliana na matakwa ya nyongeza zao Lechantre atalipwa Sh 90 milioni na Aymen atapokea Sh 45 milioni, hiyo ni tofauti kabisa na malazi, usafiri na posho zao.
Lakini katika usafiri wa ndege popote pale wanapokwenda nje ya nchi wanataka tiketi ya daraja la kwanza ambayo ni ghali zaidi ya ile ya kawaida.

Monday 28 May 2018

ADAM SALAMBA MALI YA SIMBA

Adam Saramba amesaini mkataba wa miaka miwili Simba wenye thamani ya Sh40milioni.
Straika huyo alikuwa akiwindwa pia na Yanga ambayo viongozi wake walishapeleka barua ila wakatolewa nje na lipuli.

SALAMBA RASMI SIMBA

Simba yafanikiwa kuinasa saini ya Adamu Salamba ambaye Azam FC pia ilimtaka na Yanga SC ikitaka kumtumia katika michuano ya kombe la Shirikisho la Afrika.

Huyu anakuwa mchezaji wa pili kusaini ,akiungana na Boniventure Kaheza maarufu kama Rivaldo

NJOMBE MJI NA MAJIMAJI ZASHUKA DARAJA

Ligi kuu Tanzania bara imefika tamati siku ya Leo na timu za majimaji ya Songea na NJOMBE MJI ya NJOMBE zimeshuka daraja

TANGAZO TANGAZO

Tunaomba radhi kwa kutokuweka habari mpya kutokana na sababu silizokuwa nje ya uwezo wetu

Tuesday 27 March 2018

KIMBIA MPENZI TUTAKUTANA MBELE KWA MBELE!! (Sehemu ya 11)


                                                    (the first run away love to told by Deogratius gift kipapa.)
EPISODI 11
INTRO:
Simulizi ya msichana wa shule aliyelazimika kumtorosha mpenzi wake mbali na baba yake pamoja na serikali mara baada ya kumpa ujauzito. Kamwe hakufikiri kwamba kumruhusu akimbie ni kuliruhusu penzi lake lipotelee mbali milele.  Simulizi hii, haitakuonyesha ni jinsi gani ilivyo kutengana na mpenzi wako pekee bali pia itakushangaza zaidi na uhusiano wa baba na mwana ambao kamwe hukuwahi kuuvutia picha, kuna machozi, na jasho, mbio na kuvuta pumzi, kama ulisoma simulizi yoyote ya mapenzi kutoka kwa gift kipapa na kuhakikishia ya kwamba haujasoma kitu. This is not just a heart to heart story but I run away love which no one could never ever found.
ILIPOISHIA EPISODI 10….
       “nakuja kwako , wakati , natuamaini tutakutana mpenzi wangu , na tutaishi maisha mazuri huko.”
Aliwaza pendo huku akitembea , kuelekea ilipo stendi ya mji huo, tayari ilikuwa imetimia mida ya saa kumi za alfajiri , na huo ulikuwa muda  muafaka kwa magari kuondoka kuelekea mji wa tukuyu.
Aliyakuta magari mawili na yote yalikuwa na abiria kadhaa , aliingia kwenye moja wapo na dakika kumi na tano baadae gari hilo lilianza kuondoka katika eneo hilo , na hiyo ilikuwa kwa heri ya pendo kwa mji wa itete na kwa wazazi wake pia.
MWENDELEZO WAKE:
Si kwamba ilikuwa mara yake ya kwanza kuingia katika jijiji la dare es salaam tu bali pia alikuwa hafamiani na mtu yoyote Yule anayeishi katika jiji hilo , aliposhuka ndani ya mabasi alibaki akishangaa tu, hakujua hata aanzie wapi , japo alikuwa anatembea kuufuata msululu wa abiria walioshuka pamoja nae kwenye basi, wakitoka rnje ya stendi hiyo ya ubongo.
“Tiketi iko wapi?”

JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA LAKANUSHA KUHUSIKA NA KIFO CHA KIJANA ALAIN ACHILE

                                                                                            
                                                       
TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYA HABARI “PRESS RELEASE” TAREHE 27.03.2018.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya limeendelea kukabiliana na vitendo vya uhalifu ili kuhakikisha kuwa wakazi wa Mkoa huu wanaendelea kuwa salama na mali zao. Aidha Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya limeendelea na Oparesheni na Doria za mara kwa mara ili kudhibiti vitendo vya uhalifu pamoja na kuzuia matukio mbalimbali yakiwemo ya uporaji na ukabaji na kama mtakumbuka siku za karibuni kulijitokeza vikundi vya uhalifu vilivyojiita majina ya wakorea weusi, weupe. Hata hivyo kumekuwa na matukio mawili kama ifuatavyo:-

Mnamo 24.03.2018 majira ya saa 00.15 usiku askari Polisi waliokuwa katika doria na oparesheni ya kukamata wahalifu huko maeneo ya Mtaa wa Airport ya Zamani, Kata ya Iyela, Tarafa ya Iyunga, Jiji na Mkoa wa Mbeya na katika Doria hiyo walikamatwa vijana kumi na wawili akiwemo kijana mmoja ambaye alifahamika kwa jina la ALAIN ACHILE [22] Mkazi wa Airport ya zamani.

Mtuhumiwa huyu pamoja na wenzake baada ya kukamatwa walifikishwa kituo kikuu cha Polisi Mbeya Mjini na kufunguliwa mashitaka ya UZEMBE NA UKOROFI ambapo walishikiliwa na kuhojiwa.