Thursday 21 February 2013

MAHENGE&FAMILY COMPANY LTD


MAHENGE&FAMILY COMPANY LTD
 Ni watunzaji wa mazingira na wapandaji wa miti  katika mkoa wa Mbeya wilaya Rungwe na ndio washindi wa tunzo ya Raisi kwa  mwaka 2012.pia mahenge &family company ltd wana jishughuliha na utengenezaji wa mizinga ya nyuki wa asili na utegaji wa mizinga hiyo,mpaka kufikia mwezi huu wana mizinga 280 ambayo imetegwa katika misitu mbalimbali katika kijiji cha ngumbulu.hivyo kwa kufanya hivyo kampuni imetoa ajira kwa vijana wengi wanao zunguka eneo la mradi misitu,kampuni pia imetoa miche zaidi ya elfu kumi kwa vijana hao.

KAZI ZINAZOFANYWA NA KAMPUNI
.Kuotesha miche ya miti
.Kupanda miti kwenye mashamba ya kampuni
.Kushauri na kufundisha watu wengine upandaji wa miti
.kushauri watu wasiuze mashamba na badala yake wapande miti
.kushauri watu kuto hamia mjini na badala yake waendelee kufanya kazi vijijini ambazo zitawongezea vipato
.kufundisha vijana ujasiliamali.kama vile,udereva,kupasua mbao, kukata miti kwa kutumia mashine,kuendesha pikipiki,kulima mazao mbalimbali.

JINSI WANAKIJIJI WANAVYO NUFAIKA NA MRADI
.Kutoa ajira
.Wanakijiji wana pata kuni,fito,mabanzi na mbao kutoka katika mradi wa msitu
.kampuni huwa saidia wanakijiji wakati wa matatizo mbalimbali kama vile kubeba wagonjwa na maiti kwa gari ya kampuni
 .kampuni ilitoa vitabu katika shule ya msingi ngumbulu vyenye thamani ya shilingi laki tisa na nusu.
.kampuni huji husisha na marekebisho mbalimbali ya miundombinu ya balabala pindi inapo haribika
.Pia kampuni hujihusisha na udhamini wa michezo mbalimbali,kwa kutoa jezi na mipira

Pia kampuni hii ni miongoni mwa wanabodi wa kutengeneza sheria zitakazo tumika katika nchi yetu kwa masuala ya muungano wa misitu ya watu binafsi na serikali.
Ambayo ni PUBLIC PRIVATE PARTNERSHIP[PPP]
Hivyo tunawashauri vijana waishio mijini kuacha kufanya kazi za mda mfupi [yaani kutafuta pesa asubuhi na kutumia zote jioni] Naomba tubadilike na tukumbuke kujiwekea hazina.wenye mashamba vijijini turudi tukapande miti.
 

No comments: