
Kamanda wa Polisi mkoani Iringa (RPC),Ramadhani Mungi
Na Friday Simbaya, Iringa
Mwanafunzi
 wa kidato cha pili katika Shule ya Sekondari Lugalo ameuawa kwa kukatwa
 na kitu chenye ncha kali kichwani na watu wasiofahamika kisha kupora 
pikipiki yake ambayo haijafahamika namba za usajili.
Kamanda 
wa Polisi mkoani Iringa (RPC),Ramadhani Mungi amewaambia waandishi wa 
habari ofisini kwake leo kuwa Salehe Khamis (18) aliuawa tarehe 
06/10/2014 majira ya saa 6:15 usiku katika Kitongoji cha Kikungwe 
Igumbilo, Kata ya Ruaha Manispaa ya Iringa.(Martha Magessa)
RPC alisema kuwa chanzo cha mauaji hayo ni pamoja na kuwania mali, ambapo hata hivyo, watuhumiwa wanatafutwa na jeshi la polisi.
Wakati 
huohuo, Jeshi la Polisi mkoani Iringa linamshikilia mmoja dereva wa lori
 aina ya Isuzu kwa kusababisha kifo cha mtembea kwa miguu huko katika 
Kijiji cha Itimbo Kata ya Ihimbo, Tarafa ya Kilolo mkoani Iringa.
Kamanda 
wa Polisi Mkoa wa Iringa Ramadhani Mungi alimtaja marehemu kuwa ni Linus
 Mwirafi (45) mkazi Kijiji cha Itimbo kwa kudondokewa na lori hiyo baada
 ya kupinduka.
Alisema 
kuwa gari hilo lenye namba za usajili T 244 CNK aina ya Isuzu 
likiendeshwa na Yoktani Kikula (25) mkazi wa Ipogolo lilipunduka na 
kumdondokea mtembea kwa miguu huyo na kusababisha kifo chake papo hapo.
RPC 
alisema kuwa tukio hilo lilitokea mnamo tarehe 05/10/2014 majira 
06:00hrs katika kijiji cha Itimbo wilayani Kilolo, mkoani Iringa, na 
kuongeza kuwa chanzo cha ajali hiyo ni mwendokasi na dereva amekamatwa.
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment