Monday 4 April 2016

MAGUFULI AWAAMBIA Kama wewe ni mfanyakazi, uko DC au Mkurugenzi, una wasiwasi gani?

Nimechagua safu nzuri na tutaendelea kuchaguana, wakafanye kazi. Najua wengine bado sijachagua, na wengine wanakuwa na wasiwasi.
Kama wewe ni mfanyakazi, uko DC au Mkurugenzi, una wasiwasi gani? Tena unapozidi kuwa na wasiwasi, ndiyo uwezekano wa kutolewa unakuwa mkubwa.
Ni lazima niwaambie waheshimiwa maDC, ukiwa na wasiwasi hutafanya kazi.
Na sisi tutakuona wewe hufanyi kazi. Utaondoka tu. Ukiwa Mkurugenzi ukawa na wasiwasi, huo wasiwasi ndiyo dalili nzuri ya kukufanya wewe uondoke. Fanya kazi.
Chapa kazi kwa ajili ya Watanzania hawa. Watakuona tu. Hata mimi sitakuwa Rais maisha.

No comments: