WAZIRI MEMBE AKIWA KATUMBASONGWE.
Mhe.
 Bernard K. Membe (Mb), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa 
Kimataifa akiongea na wazee waishio Katumbasongwe, kando ya Ziwa Nyasa 
ndani ya Wilayani Kyela, Mkoani Mbeya.
Wakazi wa Katumbasongwe walimiminika kwa wingi kumsikiliza Mhe. Membe.
Wazee
 wa Katumbasongwe wakinyoosha mikono kujitambulisha umri wao wakati wa 
Mkutano wao na Waziri Membe uliofanyika jana Wilayani Kyela, Mkoani 
Mbeya.  Waziri Membe alikuwa Mkoani humo kwa ziara ya siku mbili ambapo 
alitembelea maeneo na makazi ya wananchi waishio ufukweni mwa Ziwa 
Nyasa.
WAZIRI MEMBE AKIWA MATEMA
Waziri
 Membe akiongea na wakazi wa Matema, Wilayani Kyela ambapo aliwasihi 
waendelee na shughuli zao za kujiletea maendeleo.  Aidha, Mhe. Membe 
alisema Serikali inajitahidi kadri iwezavyo kutafuta suluhisho la 
mgogoro wa mpaka wa Ziwa Nyasa kati ya Tanzania na Malawi. 
Wakazi wa Matema, waishio katika ufukwe wa Ziwa Nyasa, Wilayani Kyela wakimsikiliza Waziri Membe alipowatembelea jana.
Waziri
 Membe (hayupo pichani) pia alipata fursa ya kuongea na wazee wa Matema 
ikiwa ni sehemu ya mwisho wa ziara yake ya siku mbili Mkoani Mbeya.  
Katika mazungumzo yake na wazee hao, Waziri Membe aliwaeleza kuwa ziara 
hii ni sehemu ya kukusanya ushahidi muhimu kutokana na maelezo ya 
historia watakazochangia hususan tangu enzi ya ukoloni kuhusu Ziwa 
Nyasa.






No comments:
Post a Comment