Tuesday 25 June 2013

TIMU ZAONYESHANA UMWAMBA KATIKA TAMASHA LA KUPINGA UKATILI.


Na Ibrahim Yassin, Kyela
 
TAMASHA  la uzinduzi wa mradi wa kupinga ukatili wa kijinsia uliofanyika katika uwanja wa John Mwakangale Wilayani Kyela Mkoani Mbeya umechukua sura mpya baada ya kufanyika kwa mchezo ya ngoma za asili na mpira wa miguu huku wakazi wa kyela wakipokea kwa mikono miwila uzinduzi huo.
 
Uzinduzi  huo ulifanyika jana kwa udhamini wa Shilika lisilo la Kiseikali linalojishughurisha na kupinga ukatii wa kijinsia kwa wanawake kwa kushiriana na Shilika linalolea watoto yatima na wale waishio katika mazingira magumu wilayani hapa The Mango Tree ulilenga kufungua ofisi kwa lengo la kuanza kutoa huduma hiyo katika wilaya ya Kyela.
 
Katika uzinduzi huo kulifanyika mashindano ya ngoma za asili aina ya ling”oma kati ya Ndandalo  na The amazon chaka zote za mjini ambapo ngoma zote zilitoka suruhu na kutunukiwa Kitita cha Tsh,100,000.Kwa kila ngoma.na pia kulifanyika mchezo wa kuigiza uliofanywa na kikundi cha Kasenyenda Group chini ya Comred Katering ambao walizawadiwa Tsh,100,000.kutokana na kuigiza vizuri.
 
Baada ya hapo ilipofika saa 10.30 jioni kulifanyika mpambano mkali wa kukata na shoka kwa kuzikutanisha timu pinzani kati ya stend fc na timu ya Mazombi fc,(Mavampire)katika mpambano huo lefarii wa kati alikuwa ni Ambwene Mwaipatania akisidiwa na Lain one Alliud Mwang”onda na lain two Joseph Fongo (Collina).
 
Mpira ulianza kwa kasi huku kila timu ikilisakama lango la mwenzie lakini ilikua ni timu ya Stendi fc iliyofanikiwa kupata bao la kwanza na lamwisho kwa njia ya penalt lililofungwa na Willy Mwasika Viera dakika ya 30 kipindi cha kwanza baada ya mchezaji hatari Six Mwasekaga kuchezewa rafu eneo la hatari bao lililodumu hadi daika 45 za kipindi cha kwanza.
 
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi huku kila timu ikifanya mabadiliko ili kujiboresha zaidi kwa upande wa timu ya Stendi fc  waliwatoa Fred Mido,Willy Mwasika na kuwaingiza Ally Martin na Salum Azizi, na Timu ya Mazombi fc waliwatoa Anton Maiko na Fuguto Juma na kuwaingiza Baraka Kajo na Shapy Mwakalonge.mabadiliko hayo yaliongeza mashamsham uwanjani hapo huku mashabiki wa kila upande wakupuliza mavuvuzera kutokana na mchezo mzuri.
 
Wachezaji wawili wa timu ya Mazombi Mpoki Mwakinyuke na Dulla Mwantuke walipewa kadi za njano kufuatia mchezo mchafu uwanjani hapo,huku hadi dakika 90 za mchezo timu ya Stend fc ilitoka kifua mbele kwa kuongoza goli 1.kwa 0,dhdi ya Mazombi Fc.
 
Timu ya Stendi fc walipata zawadi ya kikombe,jezi seti 1,mpira na fedha taslim Tsh,100.000.na Timu ya Mazombi walipata Kikombe kidogo,seti 1ya jezi,mpira na Fedha Tsh,50.000.zawadi zilizokabidhiwa na mkuu wa Wilaya ya Kyela Magreti Malenga ambaye alikuwa ni mgeni rasmi huku akisindikizwa na Mwenyekiti wa Halmashauri Gabriel Kipija na wenyeviti wa Serikali za mitaa na wakuu wa Idara katika Halmashaur ya Kyela.
 
Akizungumza mara baada ya Tamasha hiloMkurugenzi wa Shilika la The Mango Tree Andilile Mwambaraswa alisema kuwa lengo la kukutana ni kutamburisha mradi huo kwa jamii kwa ajili ya kupinga ukatili wa kijinsia ambao utafanyika kwa kushirikiana kwa pamoja kati ya Serikali,Asas ya The Mango tree kwa ufadhili wa Henry Jakson Foundation Medical Research Internation kupitia Water Reed na Wilaya ya Kyela imechaguliwa kuwa moja ya mfano katika utekelezaji wa mradi huu wa kupinga ukatili wa kijinsia.

No comments: