Tuesday 25 June 2013

MSICHANA KYELA AUWA ANYOFOLEWA VIUNGO SEHEMU YA MWILI


Na Ibrahim Yassin,Kyela

MSICHANA Enita Kalota (23 Mkazi wa kijiji cha Mwalisi kata ya Ngana wilayani Kyela amekutwa amekufa katika maeneo ya kijiji cha Ngana kitongoji cha Kandete kata ya Ngana huku akiwa amenyofolewa baadhi ya viungo vyake vya mwili,

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi eneo la tukio kaimu ofisa mtendaji wa kata hiyo ya Ngana Joseph Mapunda alidai kuwa ofisi yake ilipata taarifa za kuwapo mtu aliyeuawa katika kijiji hicho cha Ngana mnamo majira ya saa 3 asubuhi jana na baada ya hapo walitoa taarifa kituo kidogo cha Polisi cha Kasumulu,

Alisema msichana huyo alikuwa anaishi Boda ya Kasumulu baada ya kumaliza shule darasa la saba mwaka jana katika shule ya msingi ya Mwalisi na kuwa jana walishangazwa baada ya kuuona mwili wa msichana huyo akiwa amefia katika kijiji cha Ngana,

Mapunda alifafanua kuwa walivyoutizama mwili wa msichana huyo walikuta baadhi ya viungo vyake vikiwa havipo kama sikio na ngozi ya kisogoni vikiwa imeondolewa huku kukikwa na tetesi kuwa hata sehemu zake za siri nazo zimeondolewa

Kwa upande  wake mwenyekiti wa kijiji cha Ngana Stanley Shimwela alisema kuwa tukio hilo limewashitua sana wananchi wa kijiji hicho ukichukulia hilo ni tukio la tatu kwa mwaka huu wa 2013 ambapo vifo vyote uhusishwa na imani za kishirikina baada ya maiti zote zilizouawa kunyofolewa baadhi ya viungo vya mwili,

Mganga wa zamu katika hospitali ya wilaya Kyela aliyeufanyia uchunguzi mwili huo Dkt,Nsubiri Mwansule alisema kuwa baada ya wao kuufanyia uchunguzi mwili huo walibaini msichana huyo kupigwa na kitu chenye ncha kali eneo la kichwani kilichopelekea maumivu makali na kupelekea kifo,

Alisema kuwa hawezi kusema lolote juu ya kutokuwepo kwa baadhi ya viungo ambavyo havipo katika mwili wa marehemu kwa madai kuwa yeye si mmsemaji wa hospitali hiyo,

Kaimu mganga mkuu wa hospitali ya wilaya Dkt Apaisaria Rumisha alipotafutwa ili kulitolea ufafanuzi jambo hilo hakuweza kupatikana kwa madai kuwa yupo katika ofisi za halmashauri ya wilaya kwenye kikao.

Wananchi kwa upande wao wameiomba kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya ya Kyela kufanya juhudi za haraka za kuhakikisha wanakemea vitendo hivyo ili kuweza kupunguza vitendo hivyo vya mauaji vinavyotokea kwa imani za kishirikina vinavyoipa sifa mbaya Wilaya ya Kyela,

No comments: