Friday 2 August 2013
MAANDALIZI ya kambi la vijana walio chini ya umri wa miaka 18 yamekwisha kamilika wilayani Ileje mkoani Mbeya
MAANDALIZI ya kambi la vijana walio chini ya umri wa miaka 18
yamekwisha kamilika wilayani Ileje mkoani Mbeya ambapo yatafanyikia
Isoko kata ya Kafule kwa ya muda wa siku nne.
Akizungumza na MBEYA LEO mkurugenzi wa kambi hilo Raia Mbembela
alisema kuwa ghalama zake ni kiasi cha shilingi 570,000 katika
kulikamilisha ikiwa ni kununua vifaa vya michezo kama Mpira Jezi na
vinginevyo.
Mbembela alisema kuwa jina la timu ni Chui Akapango ambapo litakuwa
likisadifu kuacha historia katika vijana hao na kwakuwa wapo tiali
katika kushiliki kucheza mpira ili kuweza kuinua vipaji vyao.
Aliongeza kuwa dhumuni kubwa la kuinua vipaji hivyo vya watoto ni kuwa
weza kufika hadi katika vilabu vikubwa kama vile Plizoni B, Mbeya city
kwa kuwa wapo tiali kucheza kwa kujituma.
Kwa upande wake mkuu wa wilaya hiyo Rosemary Senyamule alisema
kuanzishwa kwa kambi hilo kutawasaidia wananchi wa wilaya hiyo kuwa na
kipaumbela katika michezo na hususa ni kwa vijana hao walio chini ya
umri wa miaka 18.
Senyamule aliongeza kuwa michezo ni ajila kwa vijana na ni afya pia
katika maisha ya binadamu ambapo vijana wanaweza kuondokana na tama
mbaya kama vile kunywa pombe, tamaa mbaya za mapenzi na vitendo vya
ukatili.
Katika kambi hilo mkuu wa wilaya hiyo aliwachangia vijana hao kiasi
cha shilingi 150,000 ambazo zilitumika katika kununua jezi za kuchezea
mpira.
Naye kapiteni wa vijana hao Olea Kibona alisema kuwa vijana hao wapo
tiali katika kujitoa kimchezo na kuwa wanahamo ya kuweza kwenda
kuchezea vilabu vikubwa.
Alisema kuwa vijana hao wapo tiali kucheza kwa namna yoyote ile
ilimuladi waweze kufika malengo yao waliyo kuwa wakitalajia na kuwa
wanandoto kuwa wachezaji wakubwa ambao watakuwa na moyo wa kulitumikia
taifa lao.
Mdau mwingine wa mchezo wa mpira wa miguu Injinia Laison Mkondya
alisema kuwa wapo tiali katika kufufua vipaji vya vijana hao na kuwa
wanaweza kucheza kwa kujituma.
Alisema kuwa vijana hao wanauwezo wa kucheza na kuweza kutoa hamasa
kwa vilabu vikubwa kwenda kutembelea vijijini kuliko wanapo chukua
vijana wa mjinin huku wa vijijini wakiwa wamesaulika.
Na Eliud Ngondo, Ileje
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment