KLABU
ya Manchester City imeanza na moto katika Ligi Kuu ya England chini ya
kocha mpya, Manuel Pellegrini baada ya kuifumua mabao 4-0 Newcastle
iliyomaliza na wachezaji 10 kwenye Uwanja wa Etihad usiku huu.
Mabao
ya kipindi cha kwanza ya David Silva na Sergio Aguero pamoja ya kipindi
cha pili ya Yaya Toure na Samir Nasri yalitosha kuipandisha City
kileleni mwa Ligi Kuu ya England baada ya mechi za kwanza za ligi hiyo.
Silva alifunga dakika ya sita, Aguero dakika ya 22, Toure dakika ya 50 na Nasri dakika ya 75.
Newcastle
ilipata pigo baada ya Steven Taylor kutolewa nje kwa kadi nyekundu
dakika ya 45 kwa kumchezea rafu Aguero mbele ya refa Andre Marriner.
Kikosi
cha Man City kilikuwa: Hart, Zabaleta, Kompany/Javi Garcia dk71,
Lescott, Clichy, Jesus Navas, Toure, Fernandinho, Silva/Negredo dk80,
Aguero/Nasri dk62 na Dzeko.
Newcastle: Krul,
Debuchy, Steven Taylor, Coloccini, Yanga-Mbiwa, Sissoko, Tiote,
Gutierrez/Anita dk44, Ben Arfa/Sammy Ameobi dk65, Cisse,
Gouffran/Dummett dk45.
Kula tano! Yaya Toure na David Silva wakipongezana
Mwanzo mzuri: Silva aliifungia Manchester City bao la kuongoza dakika ya sita
Kitu na boksi: Silva hakulaza damu baada ya wachezaji wa Newcastle kushindwa kuokoa krosi Edin Dzeko
Hakuna nafasi: Fabricio Coloccini na Tim Krul wakishuhudia mpira wa kichwa wa Silva ukitinga nyavuni
Kiti nyavuni: Hili lilikuwa bao la kwanza la kichwa kwa Sliva (kulia) katika Ligi Kuu England
Hapa ni namna ambavyo Silva alifunga bao lake - sasa gonga hapa kujua zaidi yaliyojiri Uwanja wa Etihad
La pili: Sergio Aguero akiifungia Manchester City na kuongoza 2-0
Kitu kinapenya: Aguero huyo
Aguero akishangilia
Chukua nyekundu: Steven Taylor alitolewa kwa kasi nyekundu kwa kumchezea
No comments:
Post a Comment