Wednesday 20 May 2015

Poroshenko amnyooshea kidole Putin



Rais wa Ukraine, Petro Poroshenko
Rais wa Ukraine Petro Poroshenko ameiambia BBC kuwa hamuamini kiongozi wa Urusi Vladimir Putin katika harakati za kuleta amani Mashariki mwa Ukraine.

Poroshenko anasema anahofia kwamba huenda kukawa na kutokuelewana kati ya mataifa hayo mawili.
Vladimir Putin
Hata hivyo ameielezea hali hiyo kuwa ni vita kamili kati ya nchi hizo.
Ameongeza kuwa awali waziri wa mashauri ya kigeni wa Marekani John Kerry alifanya mazungumzo na kiongozi huyo kabla ya mazungumzo yao na rais wa Urusi Putin.

No comments: