Tuesday 30 June 2015

Majengo ya shule ya msingi Jitengeni yabomoka wanafunzi wakatisha masomo.


Wanafunzi zaidi ya 460 katika shule ya msingi jitengeni kata ya Kihurio wilaya Same mkoani Kilimanjaro hawana mahala pa kusomea baada ya majengo ya shule hiyo kuharibiwa vibaya na upepo mkali uliosababisha baadhi ya majengo kubomoka kabisa.
Mkuu wa shule hiyo yenye wanafunzi kuanzia  shule ya awali hadi darasa la saba Bi. Nazal Abraham anasema miundombinu ya shule hiyo ni chakavu kwa madai kuwa shule hiyo ilijengwa tangu mwaka 1930 hadi sasa haijafanyiwa marekebisho licha ya wanafunzi wanendelea kutumia madarasa hayo.
 
Amesema walimu wanalazimika kutumia vyumba vitatu vyenye ufa ambavyo vimebaki kufundishi wanafunzi hao kwa awamu hali inayosababisha  elimu inayotolewa kutokidhi viwango kutokana mazingira magumu ya kufundishia.
 
Kutokana na tatizo hilo mamlaka ya elimu nchini (TEA )imetoa msaada wa shilingi milioni 30 pamoja na kuendesha harambee iliyofanikisha kupatikana kwa  kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 83.5 kwa ajili ya ujenzi wa shule hiyo ambapo mkurugenzi wa ukuzaji raslimali kutoka  tea Bi. Silivia Lupembe anasema mazingira wanayosomea wanafunzi  ni hatari.
 
Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya same Bw.Herman Kapufi ambaye aliongozana  na wadau mbalimbali kutembea shule hiyo amesema msaada wa haraka unahitajika huku baadhi ya wanafunzi  wakielezea changamoto zinazowakabili ikiwemo uhaba wa vyoo na walimu.
 

No comments: