Tuesday 30 June 2015

Takwimu za jeshi la Polisi kikosi cha usalama barabarani zinaonyesha matukio ya ajali za barabarani yamepungua.


Takwimu za jeshi la Polisi kikosi cha usalama barabarani zinaonyesha matukio ya ajali za barabarani yamepungua kwa kipindi cha mwaka 2013-2014 na kuwataka madereva wa vyombo vya moto kuendelea kutii sheria na kanuni za usalama barabarani ili kuepusha matukio ya ajali yanayoweza kuepukika.

Mkuu wa kikosi cha usalama barabarani nchini kamanda Mohamed Mpinga ameyasema hayo alipokuwa akikabidhiwa gari maalum litakalotumiwa na kikosi cha usalama barabarani katika utoaji wa elimu kwa watumiaji wa barabara kwa ufadhili wa watu wa China kwa kushirikiana na ubalozi wa China nchini Tanzania kupitia kampeni ya usalama wa barabarani ujulikanayo kama endesha kwa usalama.
 
Zoezi hilo lilifwatiwa na zoezi la utoaji wa vyeti kwa madereva wa pikipiki walio fuzu mafunzo maalum ya usalama barabara huku baadhi yao wakisema ukosefu wa elimu na kutokujitambua kwa baadhi ya madereva kunasababisha ongezeko la ajali hizo.

No comments: