Thursday 24 August 2017

Maabara ya kisasa Afrika kujengwa Tanzania


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako ameweka jiwe la msingi la ujenzi wa maabara ya Teknolojia ya Nyuklia kwenye Tume ya Nguvu za Atomiki nchini (TAEC) Arusha, maaabara ambayo inatarajiwa kuwa ya kisasa kwa vifaa Afrika.

Akizungumza na viongozi mbali mbali wa mkoa huo na watumishi wa taasisi hiyo, Waziri Ndalichako amesema maabara hiyo ni ya watanzania na hivyo watumishi wanaofanya kazi katika tume hiyo  wasifanye kazi kwa ubinafsi na badala yake watangulize maslahi ya Taifa mbele.

Majengo ya maabara hiyo ya kisasa yanatarajiwa kukamilika Februari Mwaka 2018 ambapo yatagharimu kiasi cha shilingi   Bilioni 2.3, na ikikamilika Umoja wa Ulaya itafunga vifaa vyenye thamani ya Sh. Bilioni 11 ambapo  tayari baadhi ya vifaa vya Sh. Bilioni 2.6 vimekwishawasili nchini.

Pia Waziri na viongozi wengine wa Wizara wametembela Chuo cha Veta sehemu ya kuzalishia umeme kikuletwa pamoja na Chuo cha Ualimu Elimu Maalumu Patandi, kwa lengo la kukagua miundombinu ya chuo hicho pamoja kujionea vifaa vya kufundishia wanafunzi wenye mahitaji maalumu.

Viongozi wengine ambao waliambatana na waziri kwenye ziara hiyo ni pamoja na Naibu waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia  Mhandisi Stella Manyanya na Naibu Katibu Mkuu, Profesa Saimon Msanjila

No comments: