KIINGILIO MECHI YA STARS, MOROCCO 5,000/-
Kiingilio cha chini katika mechi ya mchujo
 ya Kombe la Dunia kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Morocco (Lions of 
the Atlas) itakayochezwa Jumapili kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam 
ni sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya kijani.
 Viti
 vya kijani katika uwanja huo wenye uwezo wa kumeza watazamaji 60,000 
viko 19,648. Kwa upande wa viti vya rangi ya bluu ambavyo viko 17,045 ni
 sh. 7,000. Kiingilio kwa viti vya rangi ya chungwa ambavyo viko 11,897 
ni sh. 10,000.
 Viingilio
 vya daraja la juu ni kama ifuatavyo; VIP C yenye watazamaji 4,060 ni 
sh. 15,000 wakati sh. 20,000 ni kwa VIP B yenye watazamaji 4,160. VIP A 
yenye watazamaji 748 kiingilio chake ni sh. 30,000.
 Tiketi
 kwa ajili ya mechi hiyo itakayoanza saa 9 kamili alasiri zitaanza 
kuuzwa siku mbili ya mchezo (Ijumaa na Jumamosi) katika vituo 
vifuatavyo; Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, Sokoni Kariakoo, mgahawa 
wa Steers ulioko mtaa wa Ohio/Samora, Oilcom Ubungo, Kituo cha Mafuta 
Buguruni na Dar Live Mbagala.
 Katika
 vituo hivyo tiketi zitauzwa katika magari maalumu. Magari hayo pia 
yatafanya mauzo ya tiketi uwanjani siku ya mechi. Vilevile tunapenda 
kuwakumbusha watazamaji kutonunua tiketi mikononi mwa watu au katika 
maeneo yasiyohusika ili kuepuka kununua tiketi bandia, hivyo kukosa 
fursa ya kushuhudia mechi hiyo.
 SAMATA, ULIMWENGU WARIPOTI STARS
Washambuliaji
 wa Taifa Stars, Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu wanaochezea timu ya 
TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) wamewasili nchini 
jana usiku na kwenda moja kwa moja kambini.
 Ujio
 wa washambuliaji hao unafanya idadi ya wachezaji walioripoti kambini 
kufikia 20 kati ya 23 walioitwaa baada ya mshambuliaji Khamis Mcha 
aliyekuwa na kikosi cha timu yake ya Azam nchini Liberia naye kuripoti 
kambini leo asubuhi.
 Wachezaji
 John Bocco na makipa Mwadini Ally na Aishi Manula ambao pia nao 
walikuwa Liberia na timu yao ya Azam wataripoti kambini leo alasiri. 
Wachezaji hao ni sehemu ya msafara wa timu ya Azam ambao utakuja na 
ndege ya mchana kutokea Nairobi kwa vile ile ya asubuhi waliyotangulia 
nayo wenzao kuwa imejaa.
 
 

 
 
No comments:
Post a Comment