Wednesday 18 December 2013

TANZANIA NI NCHI YA KWANZA BARANI AFRIKA KWA SAFARI ZA UTALII , SERENGETI NA RUAHA IRINGA ZAONGOZA


 Kaimu mkurugenzi  mkuu  wa hifadhi  za Taifa (TANAPA ) Dr Ezekiel Dembe ( kulia) akimakabidhi  Bi Jane Mwakinyuke kutoka Hifadhi ya Taifa Mikumi , cheti  cha  kuhitimu mafunzo  ya mwezi mmoja ya kuongoza  watalii katika hifadhi  za Taif
Kaim mkurugenzi mkuu wa TANAPA DR Ezekiel Dembe wa pili kulia waliokaa akiwa na  kaim mhifadhi wa Ruaha Bw John Nyamhanga kulia ,Godwell ole Meing'ataki Mratibu wa mradi wa kuboresha mtandao wa maeneneo yaliyohifadhiwa kusini mwa Tanzania. ' SPANEST kushoto wa  pili na kaimu RAS Iringa pamoja na  walimu wa mafunzo  hayo na askari  waliohitimu mafunzo  waliosimama
Askari pekee wa  kike kutoka  hifadhi ya Taifa ya Ruaha Jane Griffin Mwakinyuke ambae  amehitimu mafunzo ya  kuongoza  watalii katika utalii wa miguu hifadhini akionyesha  cheti  chake

a ambao hupenda  utalii   wa  miguu  juzi ambapo  jumla ya askari 20  kutoka hifadhi mbali mbali  walihitimu  mafunzo  hayo,kulia kwake  ni Bw  Godwell ole Meing'ataki Mratibu wa mradi wa kuboresha mtandao wa maeneneo yaliyohifadhiwa kusini mwa Tanzania. ' SPANEST'(P.T)
TANZANIA  yazidi  kung'ara katika  sekta  ya  utalii barani  Afrika  baada ya kuwa nchi  ya  kwanza barani Afrika  kwa   kuvutia   zaidi  watalii katika  safari  za utalii katika  hifadhi  hiyo huku  hifadhi ya  Serengeti na Ruaha Iringa zikiongoza  kwa  ubora ya  utalii.
Kaim mkurugenzi  mkuu  wa hifadhi  za Taifa (TANAPA ) Dr Ezekiel Dembe aliyasema hayo jana  wakati  akifunga mafunzo ya mwezi mmoja ya kwa askari 20 ,mafunzo ya  utalii wa  miguu  katika hifadhi hiyo  ya Ruaha na nyingine kama Mikumi na Udzungwa   yaliyofanyika katika  hifadhi ya Taifa ya Ruaha Iringa .
Dr Dembe  alisema  kuwa Tanzania  imeonekana ni nchi ya kwanza kwa utalii  baada ya  wataalum  wa masuala ya  utalii  barani  Afrika   kuchagua  nchi nane  barani Afrika ambazo zinafaa kwa   kufanya  safari  za utalii
Alizitaja  nchi  zilizoshindanishwa  kwa  kupigiwa  kura  kuwa ni Tanzania , Botswana , Uganda , Namibia ,Afrika ya  kusini , Kenya , Zambia na Zimbabwe na   huku   Tanzania  ikionekana  ni  nchi inayoongoza kwa  safari  za kitalii  ukilinganisha na nchi nyingine  zilizowekwa katika orodha  hiyo.
Pia  alisema mbali ya kuchagua  nchi  inayofaa kwa utalii pia  wataalam hao  walitazama   maeneo  50  yaliyofaa  kwa  safari za  utalii na Tanzania ikifanikiwa kupata maeneo   10   bora zikiwemo  hifadhi  8  ambazo  zipo katika TANAPA na Selous  na Ngorongoro  huku  mlima  wa  Kilimanjaro  haukuwekwa  kutokana na hifadhi  hiyo ya  Kilimanjaro ni maalum kwa  kupanda mlima pekee.
Hata  hivyo  alisema  katika  hifadhi hizo 10 bora   kwa  hifadhi  za kusini hifadhi ya Ruaha imeongoza  ikifuatiwa na katavi  wakati hifadhi ya kwanza kwa  hifadhi  bora  ilikuwa ni  Serengeti wakati  hifadhi  ya pili  ilikuwa ni hifadhi ya Ruaha barani Afrika  ambazo  zilionekana ni  bora na  vinavutia  zaidi kwa  safari  za  kitalii.
Dr  Dembe  alisema  kuwa  hivi  sasa TANAPA  wameelekeza  nguvu  zote  katika  kuendelea  kuitangaza  hifadhi ya  Ruaha  Iringa  ikiwa ni pamoja na kubadilisha mazingira  ya  hifadhi  hiyo  ili  kuvutia  idadi kubwa  ya  watalii katika  hifadhi  hiyo ambayo  ndio  hifadhi  kubwa  kuliko  zote  katika Tanzania.
Hata  hivyo  alisema  kuwa katika  kuboresha utalii wa kusini TANAPA  ipo katika mkakati  wa  kutoa  elimu kwa madereva  wanaopeleka  wageni katika  hifadhi mbali mbali ikiwemo  hifadhi  hiyo ya Ruaha  Iringa ili  kuona kampuni za kitalii kuwa na madereva ambao wanajua  vema  utalii na kuepuka  udereva  wa  vurugu katika  hifadhi.
Alisema  kuwa utalii ni  sekta  nyeti katika  Taifa  hivyo  lazima wale  wote  wanaohusika na masuala ya utalii kuwa na elimu ya  kutosha  juu ya utalii na  kuyataka makampuni kuepuka  kuwatumia madereva wa daladala kupeleka  wageni  hifadhini ambao baadhi yao  wamekuwa hawana elimu ya utalii .
Kuhusu askari  hao  20  waliopewa mafunzo  Dr Dembe  aliwataka  kuwa wazelendo  na hifadhi pamoja  na Taifa  zima la Tanzania  na kuepuka  kugeuka  kuwa maadui  wa  hifadhi kwa kushirikiana na majangili  kuhujumu  hifadhi  hizo .
Wakati  huo  huo Dr Gembe  alivitaka  vyombo  vya habari na wanahabari  nchini  kuendelea  kutangaza  utalii ikiwa ni pamoja na  kuepuka  kuandika habari  ambazo  hazisaidii katika ukuzaji  wa sekta ya utalii .
Alisema  iwapo  vyombo  vya habari  nchini  vitafanya  vizuri  katika  kuhamasisha  utalii na  kuwa na uzalendo  na Taifa la Tanzania katika kuepuka  kuandika habari  za kutisha  wageni kufika katika  hifadhi ni  wazi sekta ya utalii nchini haitakuwa .
Kaimu  mhifadhi mkuu wa hifadhi ya Ruaha  Bw  John  Nyamhanga  mbali  ya kuomba TANAPA  kusaidia  kumaliza kero ya  vitendea kazi kwa askari hao  bado   alisema  kuwa  mafunzo  hayo ya utalii  wa miguu kwa askari  hao ni mzuri  zaidi  japo  mafunzo  hayo yanaweza  kukwamisha upande mmoja katika utendaji kazi  wa kila  siku  katika hifadhi  hiyo ya Ruaha .
Kwani  alisema  kuwa askari  hao  ndio ambao  wamekuwa  wakitumika katika  shughuli nyingine za hifadhi  hiyo  hivyo iwapo TANAPA haita ongeza idadi ya  watumishi  wengine  kuna  uwezekano  wa kupunguza idadi  ya  watumishi  wa  idara  nyingine .
Godwell ole Meing'ataki Mratibu wa mradi wa kuboresha mtandao wa maeneneo yaliyohifadhiwa kusini mwa Tanzania. ' SPANEST alisema  kuwa  lengo la SPANEST  ni  kuendelea  kuboresha  zaidi hifadhi  ya  Ruaha ni nyingine ili  kuwavutia  zaidi  watalii wa ndani na nje  kufika katika  hifadhi  hizo .

No comments: