Monday 15 April 2013

AFISA MTENDAJI KYELA AKALIA KUTI KAVU.

 
KIKAO Cha dharura  cha baraza la madiwani kilichoketi mwishoni mwa wiki iliyopita kilimtaka Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Kyela Mkoani Mbeya kumfikisha mahakamani Afasa mtendaji wa kijiji cha Ipinda Boniface Kayuni kutokana na kosa la wizi wa feddha linalomkabili.

Akizungumza  katika kikao hicho mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya Gabriel Kioija alisema Afisa huyo anayetuhumiwa kwa kosa la kufoji kaboni sleep katika risiti na kujipatia fedha Tsh,3,42,000 kinyume cha taratibu huku akiikosesha mapato Halmashauri,

Kipija  alisema kuwa kutokana na kosa hilo Halmashauri iliunda tume kwa lengo la kuchunguza tuhuma hizo ambapo tume hiyo ilibaini ukweli wa kosa hilo na kupeleka vielelezo hivyo kwenye baraza hilo ambalo tayari limemtaka Mkurugenzi huyo ampeleke mahakamani ili sheria ichukue mkondo wake,

‘’Kutokana na ushahidi na nvielelezo tulivyovipata kutoka katika tume ya uchunguzi umeonekana kuwa Afisa huyo mtendji amekuwa na tabia ya kutenda kosa kama hilo mara kwa mara na kujipatia fedha kinyume na taratibu huku akiikosesha fedha Halmashauri hivyo sisi kama madiwani hatuko tayari kufanya kazi na mtu wa namna hiyo,tunakuamuru mkurugenzi umpeleke mahakamani ili sheria ifanye kazi yake,’’alisema Kipija,

Aliongeza kuwa watendaji katika Halmashauri ya Kyela wamegeuka midomo ya mamba kwa kutafuna fedha za umma zinazotokana na michango mbalimbali hivyo wao kama madiwani hawatakuwa na huruma na watu kam hao,

Afisa mtendaji wa kijiji hicho cha Ipinda Bonifasm Kayuni anayetuhumiwa kwa kosa hilo,mbari na kukiri  kuwepo na kosa hilo aliomba msamaha na kudai kuwa waliomsababishia kosa hilo ni  wasaidizi  wake na kwamba kwa kuwa yeye ni afisa mtendaji wa kijiji husika na kosa limeonekana kwake hivyo aliomba msamaha ambapo msamaha huo uligonga mwamba,

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Kyela Abdarah Mfaume kwa upade wake alisema kuwa ndiyo Afisa mtendaji huyo amekutwa na hatia na kwamba sheria za
Kazi zinasema mtumishi akikutwa na hatia inatakiwa ashushwe cheo au afukuzwe kazi na wao walifuata sheria hiyo ya kumfukuza kazi kwa kuwa cheo alicho kuwa nacho ni cha chini,

Aliongeza kuwa kutokana na afisa huyo kuwa na cheo cha chini waliazimia kumfukuza kazi kitendo kilicho pingwa na madiwani ambao wametoa pendekezo la kumfikisha mahakamani ili hatua zaidi za kisheria zifuatwe ili iwe fundisho kwa watendaji wengine wabadhirifu na  yeye amefuata agizo hilo ambapo tayali mtuhumiwa amefikishwa katika vyombo hivyo vya kisheria,

‘’Baada  ya tume kuleta majibu na yeye kukili kosa sisi kama waajiri tuliazimia kumfukuza kazi kutokana na kanuni ya sheria za kazi,lakini madiwani wametaka afikishwe mahakamani kwa hatua zaidi ambapo sisi tumefuata agizo la madiwani kwa kuwa ndio wenye Halmashauri,’’alisema Mfaume,

Mfaume alisema kuwa  pamoja na kuazimia kumfukuza kazi  afisa mtendaji huyo kwa kosa alilolitenda  tayari amefikishwa  katika vyombo vya sheria kama walivyotaka madiwani.

 Na Ibrahim Yassin,Kyela

No comments: