Tuesday 4 November 2014

ASAKWA NA POLISI KWA TUHUMA ZA KUMCHINJA MWANAMKE MWENYE UMRI WA MIAKA 65, HUKO MUFINDI-IRINGA



Kamanda wa jeshi la Polisi mkoani Iringa, Ramadhani Mungi alisema tukio hilo limetokea juzi katika kijiji cha Bumilayinga, na kumtaja mwanamke aliyeuawa kuwa ni  Maurisia Malangalila (65).Alisema kuwa sababu za mauaji hayo ni imani za kishirikina.
 Kamanda Mungi aliongeza kuwa kutokana na mauaji hayo, jeshi hilo linamtafuta mkazi wa kijiji hicho Patrick Ngerenge ili achukuliwe hatua za kisheria kwa madai kuwa alikimbia baada ya tukio hilo.
 Hata hivyo, Mungi alisema  kuwa mtuhumiwa huyo atafikishwa mahakamani ili kujibu tuhuma zinazomkabili baada ya kutiwa mbaroni.

No comments: