Sunday 10 May 2015

DUNIA KUJADILI CHANGAMOTO NA ATHARI YA MADAWA YA KULEVYA



Bw. Sam Kutessa, Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.
Na Mwandishi Maalum,
New York
Jumuiya ya Kimataifa inajiaanda kwa mkutano maalum na wa aina yake kufanyika, ambapo nchi wanachama watakutana na kujadiliana kwa kina kuhusu changamoto na adhari kubwa zitokanazo na biashara haramu na matumizi ya dawa za kulevya.
Mapema wiki iliyopita, wajumbe wanaoziwakilisha nchi zao hapa Umoja wa Mataifa, walikuwa na mkutano wa siku moja ambao ulikuwa ni sehemu ya maandalizi ya mkutano huo maalum utakaofanyika mwezi Aprili 2016.
Mkutano huo wa maandalizi uliofanyika hapa Umoja wa Mataifa na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wakiwamo mawaziri kadhaa kutoka nchi hasa za Amerika ya Kati ambako nchi nyingi zinakabiliwa na changamoto kubwa ya biashara hiyo, uliandaliwa na Bw. Sam Kutessa, Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.
Katika majadiliano ya mkutano huo , ilidhihirika wazi kwamba hakuna nchi hata moja duniani iwe tajiri au maskini ambayo haijakumbwa na janga la biashara na matumizi ya dawa za kulevya.
" Hakuna nchi ambayo imepona kutokana na biashara hii yenye thamani ya mabilioni ya dola. Licha ya juhudi kubwa na raslimali nyingi ambazo mataifa yanatumia kukabiliana na janga hili, lakini tatizo linaendelea kukua" akasema Bw. Sam Kutessa wakati akifungua mkutano huo.

No comments: