Monday 15 July 2013

MAN UNITED YAWEKA MEZANI CAMP NOU PAUNI MILIONI 26 KWA AJILI YA FABREGAS..HIZO NI HASIRA ZA KUMKOSA ALCANTARA


KLABU ya Manchester United imepiga hatua katika harakati zake za kutaka kumsajili Cesc Fabregas baada ya Mashetani hao Wekundu kuweka mezani Pauni Milioni 26 kwa ajili ya kiungo huyo wa Barcelona.
Timu ya David Moyes imekuwa ikihusishwa na mpango wa kutaka kumsajili Nahodha huyo wa zamani wa Arsenal, ambaye amekuwa akipambana kuwa mchezaji muhimu kwa mabingwa hao wa Hispania.
Lakini baada ya kumkosa mchezaji mwenzake wa Barca, Thiago Alcantara kufuatia nyota huyo wa timu ya taifa ya Hispania chini ya umri wa miaka 21 kuamua kujiunga na Bayern Munich, tmabingwa hao wa Ligi Kuu England sasa wako tayari kutumia fedha zaidi kuhakikisha mwanasoka huyo wa kimataifa wa Hispania anarejea England.
Heading back to England? United have offered Barcelona £26m for Fabregas
Anarudi England? United imeipa Barcelona ofa ya Pauni Milioni 26 kwa ajili ya Fabregas
Klabu ya zamani ya Fabregas, Arsenal inaweza kupiga bao katika dili ikitaka, kutokana na The Gunners kupewa kipaumbele cha kumsajili mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26.
Mtendaji Mkuu wa United, Ed Woodward hivi karibuni amesema kwamba klabu iko tayari kushindana kugombea wachezaji hata kwa dau la Pauni Milioni 60 hadi 70 na kwamba wanataka kusajili wachezaji wakubwa duniani.
Smart: Fabregas arrives with girlfriend Daniella Semaan at Barcelona team-mate Xavi's wedding on Saturday
Mtanashati: Fabregas akiwasili na mpenzi wake Daniella Semaan katika harusi ya mchezaji mwenzake wa Barcelona, Xavi Jumamosi
Ofa ya United kwa Fabregas ni pungufu ya kiasi cha Pauni Milioni 5 kufika dau la Pauni Milioni 30.75 ambalo linashikilia rekodi ya mchezaji wa bei mbaya kusajiliwa na klabu hiyo, walipomnunua mshambuliaji wa Tottenham, Dimitar Berbatov mwaka 2008.
Fabregas alitimkia Barcelona akitokea Arsenal kwa Pauni Milioni 31 mwaka 2011, lakini licha ya kuonyesha soka nzuri amekuwa akipambana ili kuwa mchezaji tegemeo wa kikosi cha kwanza akiwa na klabu hiyo ya La Liga.
Red Devils? Fabregas (left) and Robin van Persie could be reunited following their spell at Arsenal
Mashetani Wekundu? Fabregas (kushoto) na Robin van Persie wanaweza kuungana tena baada ya kuachana Arsenal
Ikiwa kiungo huyo atakwenda Old Trafford, ataungana na mchezaji mwenzake wa zamani wa Arsenal, Robin van Persie, ambaye alicheza na Mholanzi huyo Kaskazini mwa London kati ya mwaka 2004 na 2011.
Mspanyola huyo ambaye alianzia soka ya ushindani kwa Washika Bunduki wa London na kucheza jumla ya mechi 212 za Ligi Kuu, akifunga mabao 35 na kutoa pasi za mabao 70 sasa ni mmoja wa wachezaji wakubwa Ulaya.

No comments: