Tuesday 5 May 2015

Serikali imeagiza wananchi ambao wamejenga nyumba kuzunguka mgodi wa North Mara kuzibomoa


Serikali imeagiza wananchi wote ambao wamejenga nyumba kuzunguka mgodi wa North Mara kuzibomoa mara moja nyumba hizo kabla ya serikali haijachukua hatua.

Serikali imeagiza wananchi wote ambao wamejenga nyumba kuzunguka mgodi wa North Mara baada tu   ya kufanyika kwa tathimini ya mwaka 2011 kwa lengo la kutaka kulipwa fidia na mwekezaji kampuni  ya ACACIA  MINING kuzibomoa mara moja nyumba hizo kabla ya serikali haijachukua hatua ya   kubomoa ili kutokwamisha mipango mbalimbali ya uendeshaji wa mgodi huo.
 
Agizo hilo la serikali limetolewa na naibu waziri wa nishati na madini anayeshughulika sekta ya  madini Mh.Charles Kitwanga,baada ya kutembele baadhi ya vijiji na kushuhudia maefu ya nyumba   maarufu kama tegesha ambazo zimejengwa ndani ya miezi mitatu tu baada ya zaoezi la tathimini  kukamilika kwa lengo la kutaka kulipwa fidia kubwa,ambapo ametumia nafasi hiyo kuwataka  wananchi le ambao tayari wamefanyiwa tathimini kupokea fidia yao na kupisha katika maeneo hayo.
 
Akito maelezo kwa naibu waziri huyo wa nishati na madini,meneja uendelezaji wa mgodi wa North  Mara Bw. Abel Yiga,amesema awali walikusudia kuufunga mgodi huo kutokana na changamoto hiyo   ya uvamizi wa maeneo hayo baada ya tathimini ya mwaka 2011 kuonyesha kuwa kiasi cha shilingi  bilioni tano kilitajika kulipwa kama fidia lakini baada ya ujenzi huo kufanywa kinyume na taratibu inahitaji kiasi cha shilingi bilioni 40 ili kulipa fidia hiyo.
 
Hata hivyo baadhi ya wananchi na viongozi wa vijiji hivyo,wamekiri kuwa tatizo la umasikini ni  moja ya sababu ambayo iliwafanya kujenga majengo hayo lengo la kushawishi kulipwa fidia kubwa  hivyo wameiomba serikali na uongozi wa mgodi kukubali kutoa fidia  kwa wananchi wanaomiliki maeneo hayo kabla ya kufanyika zoezi la  tathimini ya mwaka  2011. 
 

No comments: