Friday 17 July 2015

Vyama vya siasa Zanzibar vyasaini makubaliano ya maadili ya uchaguzi mkuu.


Pamoja na mvutano mkubwa ulioibuka kutoka kwa vyama vya siasa na tume ya uchaguzi ya Zanzibar hatimaye vyama hivyo vya siasa vimesaini makubaliano ya maadili ya uchaguzi mkuu.
Mvutano huo uliibuka baada ya viongzoi wa vyama hivyo vya siasa kukataa kusiani makubaliano hayo kwa madai ya kutokuwepo kwa wawakilishi wa CCM na jeshi la polisi hali iliyosababisha mabishano na kutaka kikao hicho kiahirishwe hadi CCM na polisi wawepo katika zoezi la uwekaji saini.
 
Hata hivyo baada ya mwakilishi wa CCM kutokozea na bado zoezi hilo lilikuwa gumu mbapo ukosefu wa polisi ndio sababu nyengine lakini baada ya mabishano makali huku vyama vyingine kutishia kuondoka, wawakilishi hao wa vyama walikubali kusaini baada ya busara za mwenyekiti wa kamati ya maadili Bw Nassor Khamis huku kamati hiyo ikiahidi kuhakiksha jeshi hilo linaweka saini hiyo baadae.
 
Akizungumza baada ya kumalizika zoezi hilo mwenyekiti wa tume ya uchaguzi Bw Jecha Simai Jecha aliwahakikshia viongzoi wa vyama hivyo ZEC itatekeleza wajibu wake na uadilifu mkubwa huku mwaklishi wa UNDP ambao ndio wafadhili wakubwa wa ZEC kuwataka viongozi wa vyama hivyo kuyaheshimu maadili na makubaliano hayo.
 
Baadhi ya makubaliano yaliyosainwa na vyama hivyo 22 vya siasa ni kuhakisha kampeni za ustarabu, kuepukana na matusi na kuheshimiana na kufuatwa kwa sheria za nchi.
 

No comments: