Thursday 14 February 2013

Mwanariadha Oscar Pistorius amuua mpenzi wake kwa risasi. “Valentine’s Day surprise that went tragically wrong”.




 Mwanariadha Oscar Pistorius alipokuwa katika mashindano ya Olympic mwaka 2012 mjini London.
Mwanariadha na mshindi wa medali za dhahabu wa Paralympic raia wa Afrika Kusini, Oscar Pistorius, amekamatwa  nyumbani kwake mjini Pretoria kwa kosa la kumuua mpenzi wake baada ya kumpiga risasi moja kichwani na nyingine mkononi , majeraha yaliyopelekea kifo cha binti huyo.

Chanzo cha Pistorius kumsuti mpenzi wake bado hakijaeleweka, japo fununu za awali zinadai uenda Pistorius alijichanganya na kudhani amevamiwa na mwizi/jambazi kutokana na hali mbaya ya uhalifu anayoikabili nchi ya Afrika Kusini.

Binti huyo Reeva Steenkamp, (30) mwanamitindo alilenga kumsuprise Pistorius kwaajili ya valentine.

Msemaji wa Polisi aliliambia shirika la habari la Reuters “tumekuta pisto ya mm9 eneo la tukio, na mtuhumiwa amepelekwa kituoni kwaajili ya utaratibu mwingine”.

Pistorius mwenye miaka 26 maarufu kama “blade runner” amekuwa ni mlemavu wa kwanza kushiriki Olympic mbali na mashindano yao maalum ya Paralympic , hukimbia riadha kwa kutumia vifaa maalum vilivyofungwa miguuni kwake,  baada ya kuzaliwa bila miguu yote miwili.
 
Mpenzi wa Pistorius, Mwanamitindo  Reeva Steenkamp aliyepigwa risasi na kupoteza maisha.
 Oscar Pistorius akiwa na mpenzi wake   Reeva Steenkamp November 2012.

No comments: