CHAMA Cha
 Mapinduzi (CCM) kimesema kauli ya Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia 
na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa kwamba kuna baadhi ya 
watumishi wa vyombo vya dola wanaripoti kwake, kimesababisha baadhi ya 
wananchi kukosa imani na vyombo hivyo.
Kauli 
hiyo ilitolewa jana na Mkoa Maalum wa CCM Dar es Salaam baada ya kikao 
chao kutathimini mambo na matukio mbalimbali yanayolitikisa taifa kwa 
sasa.
Katika 
taarifa yao iliyosainiwa na Katibu wa Wilaya ya Dar es Salaam (ya 
kisiasa - CCM), Daniel Zenda ilisema kuwa Dk. Slaa amekuwa akitoa kauli 
hizo mara kwa mara tangu wakati wa kampeni za urais mwaka 2010, lakini 
hajaitwa kuulizwa wala kuchukuliwa hatua.
“Lakini
 pia kauli ya Dk. Slaa imesababisha wananchi wakose imani na Idara ya 
Usalama na zaidi kupoteza imani juu ya uwezo wa serikali kuwalinda na 
kuwahakikishia usalama wa maisha yao, ambapo ni jukumu la kikatiba la 
serikali,” ilisema taarifa hiyo.
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment