Thursday, 5 September 2013

VAN PERSIE AKANA KUMKUMBUKA FERGSUON, ASEMA MOYES POA SANA TU



MSHAMBULIAJI Robin van Persie amepuuza tetesi kwamba hafurahii maisha chini ya kocha mpya Manchester United, David Moyes.
Taarifa za Daily Star na Metro zilisema kwamba van Persie amewaambia rafiki zake anamkumbuka kocha wa zamani wa United, Sir Alex Ferguson, na Mholanzi huyo amesema hashawishiki na ufundishaji wa Moyes.
Van Persie alifurahia matunda katika mechi ya kufungua msimu, akifunga mabao mawili katika mechi ya Ngao ya Jamii dhidi ya Wigan kabla ya kufunga tena mawili katika ushindi wa United wa 4-1 dhidi ya Swansea.
Van Persie Moyes
Mholanzi: Robin van Persie (katikati kushoto) ameshindwa kufunga kwenye Ligi Kuu chini ya kocha mpya, David Moyes
Robin Van Persie
Amepagawa: Mholanzi huyo hakufurahia matokeo dhidi ya Liverpool
Pamoja na hayo, mshambuliaji huyo alishindwa kufurukuta katika sare ya United ya 0-0 nyumbani dhidi ya Chelsea kipigo cha 1-0 dhidi ya Liverpool.
Van Persie alionekana kuchanganyikiwa na hali ya mambo Anfield, na Mholanzi huyo alilimwa kadi ya njano na angeweza kutolewa nje kwa kadi nyekundu kilaini baada ya kupambana na Nahodha wa Liverpool, Steven Gerrard.
Lakini Van Persie, aliyefunga mabao 30 United msimu uliopita, amesema anafurahia zama mpya Old Trafford.
Van Persie Gerrard
Chupuchupu nyekundu: Van Persie alikuwa ana bahati kutoonyeshwa kadi nyekundu baada ya kumchezea rafu Gerrard (katikati)
Van Persie Ferguson
Baba: Kuna madai kwamba Van Persie anamkumbuka Ferguson, kocha aliyemnunua United
Aliliambia De Telegraaf: "Ni babu kubwa kufanya kazi na kocha mpya David Moyes. Ninafurahia mtindo wa Moyes. Anafanyisha mwenyewe mazoezi; yupo karibu na wachezaji na anatuandaa na kutupa maelekezo vizuri kwa mchezo dhidi ya wapinzani wafuatao. Ambayo inatuweka vizuri,".
"Kuna hali nzuri ya kufurahisha katika klabu. Taji la mwaka jana limetupa njaa zaidi ya mataji,"alisema.

No comments: