MABINGWA watetezi wa ligi kuu soka Tanzania bara, Klabu ya Yanga, wamewafagilia wanandinga wao kwa kutekeleza majukumu yao na ndio maana wanafanya kazi kubwa kuhakikisha wanatetea taji lao walilotwaa msimu uliopita, huku wakimaliza ligi kuu kwa kuwateketeza watani wao wa jadi, Simba SC kwa mabao 2-0.
Afisa habari wa klabu hiyo Baraka Kizuguto amesema kuwa kwa sasa wanaendelea na mazoezi ya kujipanga
kuelekea mchezo wa septemba 14 dhidi ya Mbeya City katika uwanja wa
kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya.
“Yanga
ndio mabingwa watetezi, washindi wa kikombe cha ngao ya jamii, mabingwa
watarajiwa wa ligi kuu msimu huu, hivyo kazi ni moja tu, tunapambana na
kujipanga kufanya vizuri zaidi, na kikubwa kinachotia moyo ni uwezo
mkubwa wa kikosi na morali ya hali ya juu”. Alisema Kizuguto.
Mechi
iliyopita, Yanga walikabwa na Wagosi wa Kaya na pichani juu, Ally
Mustafa ‘ Batez’ golikipa wa Yanga akijaribu kumhadaa nahodha wa Coastal
Union, Jerry Santo kabla hajapiga penati katika matokeo ya sare ya 1-1
Kizuguto
ameongeza kuwa wanatambua Mbeya City imekuja kwa nguvu sana, lakini kwa
Yanga bado sana na lazima cheche zao zitazimwa tu wakiwa nyumbani kwao.
Pia
amewataka mashabiki wa Yanga, nyanda za juu kusini kujitokeze kwa wingi
kuwaona mabingwa watetezi kwani burudani kubwa itaonekana.
“Yanga
ni timu ya wananchi, na kila inapocheza mashabiki wanajitokeza kwa
wingi, hivyo tunaendelea kuwaomba wazidi kujipanga kuelekea kipute
hicho”. Alijigamba Kizuguto.
Kikosi
cha Mbeya City kilichotoka suluhu (0-0) na wakali wa Kagera Sugar
kutoka Kaitaba katika mechi ya ufunguzi wa ligi kuu soka Tanzania Bara,
Agosti 24 Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya
No comments:
Post a Comment