Wednesday 27 May 2015

Watu elfu 36 wanasadikiwa kuwa na ugonjwa wa vikope –Trakoma- katika mkoa wa Mtwara.


Watu elfu 36 wanasadikiwa kuwa na ugonjwa wa vikope –Trakoma- katika mkoa wa Mtwara, huku baadhi yao wakigoma kupatiwa matibabu kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo ukosefu wa elimu juu ya athari ya ugonjwa huo ambao husababisha upofu wa macho.
Akizungumza katika uzinduzi wa programu maalumu ya miaka minne iliyofanyika wilayani Masasi kata ya Namatutwe kaimu mganga mkuu wa mkoa Mohamed Kodi amesema katika kata tano za wilaya ya Masasi wanachi 260 walijitokeza kupata huduma hiyo kati yao 112 waligoma kusafishwa macho jambo ambalo linarudisha nyuma kampeni hiyo ya kutokomeza ugonjwa huo.
 
Amesema mkoa wa Mtwara unawagonjwa wapatao elfu 36 huku wilaya ya Masasi ikiwa  na wagonjwa wa vikope wapatao elfu tisa hivyo ametaka wananchi hao kutoa ushirikiano ili kupata tiba hiyo ambayo ni bure.
 
Hata hivyo baadhi ya wananchi wametaka serikali kutoa elimu kabla ya kuleta matibabu ili yafanikiwe kuliko ilivyo hivi sasa ambapo serikali inatumia gharama kubwa kufanikisha kampeni hiyo pasipo kuelimisha juu ya umuhimu wa tiba hiyo kwa walengwa.

No comments: