Friday 4 October 2013

AJALI MBAYA MLIMA KITONGA,

 

Ajali mbaya  nyingine  imetokea  usiku  huu katika mlima kwa Kitonga wilaya ya Kilolo mkoani Iringa katika barabara  kuu ya Dar es Salaam -Iringa .
Katika  ajali  hiyo  watu  wawili wamekufa papo hapo huku wa wawili  wakijeruhiwa  vibaya baada ya malori mawili kugongana  uso kwa uso .

Ajali  hiyo imetokea  mida ya saa 12.50 jioni   ikiwa ni dakika takribani 30  baada ya ajali ya basi la JM kupinduka eneo  la Mazome  wilaya ya Kilolo.

waliopoteza maisha katika ajali  hiyo ambayo chanzo ni dereva  wa lori la IT lililokuwa  likisafirishwa kwenda nchi  za  kusini mwa Tanzania aliyekuwa akitaka  kulipita gari la mbele mlimani na katika kona kali .

Hata  hivyo  dereva  wa  lori  hilo IT aliyetambuliwa kwa jina la Gody  amevunjika mguu  wake ambao umetoka katika na  dereva  na utingo la fuso wamekupa papo hapo  huku mwanamke  aliyekuwa katika lori IT akisalimika .

No comments: