Friday 4 October 2013

DOLA ZA KIMAREKANI 31 MILIONI KUTUMIKA KATIKA UJENZI WA BARABARA YA LWANJILO HADI CHUNYA

 

MRADI wa kutengeneza barabara ya lami kutoka Lwanjilo mpaka Chunya utaigharimu Serikali ya Tanzania dola za Kimarekani zipatazo milioni 31, sawa na shilingi bilioni 40.2 za Kitanzania.

Kauli hiyo imetolewa hivi karibuni na meneja mradi wa kampuni ya ujenzi ya China Communications Construction Company Limited ya Nchini China, Xia Fei, alipokuwa akizungunza na waandishi wa habari ofisini kwake katika kijiji cha Chalangwa, wilayani chunya.

  Alisema mradi huu ambao utagharamiwa na serikali ya Tanzania utachukua jumla ya miezi 27 kuumaliza, ambacho ni kipindi cha miaka 2 na miezi 3.

Hata hivyo meneja huyo ame sema kuwa shaka yao kubwa ni kipindi cha masika ambacho kinakaribia, na ambacho amekielezea kuwa kitasababisha kazi kuwa ngumu kutokana na mvua.
Alisema kazi imekuwa ikienda taratibu kutokana na serikali kuchewesha kuwalipa fedha za ujenzi, ambapo aliongeza kuwa fedha zimekuwa zikitolewa katika mafungu na hivyo kusababisha kazi ya ujenzi kuchelewa kwenda na wakati.

Fei alisema kuwa awali serikali ilitakiwa kuwalipa asilimia 15 ya fedha zote za ujenzi shilingi bilioni 6.2 za kitanzania, kutoka katika fedha zote za mradi wa ujenzi wa barabara hiyo yenye urefu wa kilomita 36 ambazo ni shilingi bilioni 40.2.

Alisema badara yake mwanzoni kabisa serikali ilitoa fedha kidogo ambazo ni bilioni 1.2 zilitolewa Oktoba 2009, na ilipofika Disemba mwaka huo huo serikali iliongeza fungu linguine la shilingi bilioni 2.23.
Aliongeza kuwa kwa mara ya tatu Juni 2010 serikali ilitoa tena shilingi bilioni 1.7, na ilipo fika julai mwaka huohuo selikali ilitoa shilingi bilioni o.841 ili kuendeleza ujenzi wa barabara hiyo.
Meneja mradi huyo alisema kuwa pamoja na kwamba serikali imetoa maripo kidogo kwa kuchelewesha na bira kufuata mda lakini kampuni yake ya CCCC wanafanya kazi kwa bidii, ili waweze kumaliza kazi mapema ifikapo mwakani.

Alisema kuwa mpango nzima na kitu muhimu katika mradi wa barabara hiyo ni kumaliza ujenzi wa kilomita 36, pamoja na ujenzi wa madaraja makubwa manne na makaravati zaidi ya 30.
Fei alisema kuwa mpaka sasa kampuni hiyo imekamilisha ujenzi wa kilomita 11.1 kwa kiwango cha lami na kubakia kilomita 24.9 ambazo wanatarajia kuzikamilisha mapema mwakani.

Hivi karibuni Waziri wa Ujenzi, John Magufuli alitembelea eneo la mradi kukagua maendeleo ya ujenzi ambapo aliridhika  na kufurahishwa na ubora wa kazi unao fanywa na kampuni hiyo ya wachina.
Waziri Magufuli aliwapongeza wachina kwa kazi nzuri wanayo fanya na kuwahimiza kufanya kazi kwa bidii, ili kufikia malengo ya kuimariza kazi hiyo mapema kabla ya kuikabidhi rasmi kwa serikali.
Hata hivyo waziri huyo wa ujenzi alionya kuwa endapo kampuni hiyo ya wachina itashindwa kumaliza kazi mapema kamawalivyo kubalina, serikali haitasita kukatisha mkataba na kuto walipa fedha zao.

No comments: