Friday 4 October 2013

WATATU WAHUKUMIWA KIFO




MAHAKAMA kuu kanda ya Mbeya imewahukumu kunyongwa hadi kufa watu watatu wakazi wa tukuyu wilayani Rungwe,wakituhumiwa kwa makosa ya mauaji .
Katika kesi ya kwanza jaji Samweli Karua wamahakama kuu kanda ya Mbeya iliyohamishia shughuli zake katika mahakama ya wilaya ya Rungwe,imemtia hatiani na kumhukumu kunyongwa hadi kufa mshtakiwa Rashidi Mwanyerere baada ya kukutwa na hatia ya kumuua  kwa makusudi baba yake mdogo.
Akisoma hukumu Mahakamani hapo Jaji Karua amesema mhutuhumiwa anatiwa hatiani pasipo shaka kutokana na ushahidi wa mazingira ambayo mtuhumiwa alimkata na panga marehemu shingoni nakiisha kumwagia maji ya moto ili kusudi kuzuia damu isimwagike .
Katika kesi ya pili Jaji Kalua amewahukumu kunyongwa hadi kufa watuhumiwa wawili akiwemo mwanamke kwa kosa la kumbaka kiisha kumuua mtoto mwenye umri wa miaka mitatu na nusu,watuhumiwa hao ni Mage Kalamu[45]na Ezekia Nassoro Matatu[43]ambao kwapamoja na kwa makusudi walimuua mtotpo Edina Daudi kwa kumbaka na kumnyoga shingo.
Watuhumiwa walikutwa na hatia kutokana na majigambo ya mtuhumiwa wa kwanza Mage Kalamu kwamba pesa zilizo patikana kutokna na kumuua marehemu zilikuwa ndogo hakuwa nasoko kwani walimuuza kwa shilingi milioni mbili na nusu.
Kutokana na ushahidi huo Jaji Karua amewahukumu kunyongwa hadi kufa watuhumiwa wote wawili kutokanana kushindwa kujitetea wala kujibu lolote mahakamani hapo.  
                 Na SARA ZAKAYO

No comments: