
Sasa ni rasm, Bw Maiko Litanda aliyekuwa kiongozi wa kundi la M4U,
lililokuwa likimuunga mkono mbunge wa Monduli Edward Lowasa anasema
maamuzi yaliyofanywa kwa manufaa ya wachache ndani ya CCM kwa kumkata
jina Bw Edward Lowasa wanasema hawakati tamaa na kwamba safari yao ya
matumaini bado inaendelea na sasa inahamia chama cha Democrasia na
maendeleo Chadema.
Kwa mujibu wa kiongozi huyo wa M4U anasema zaidi ya viajana 100
wamekwisha kujiunga na Chadema ambapo imeshuhudia kad 50 pekee za
viajana hao, huku uongozi wa Chadema mkoa ukiwahakikisha kuwafikisha
salama katika safari ya matumaini.
Katika hatua nyingine chama cha ACT wazalendo kimepokea wanachama 7
kutoka vyama vya upinzani ambapo wanadai kuondoka kwao kunatokana na
viongozi wa vyama hivyo kuwa na ombwe la uongozi huku vingine
vikiendeshwa kwa ukanda.
Vugu vugu hili linakuja siku kadhaa zikiwa zimesalia kabla ya Ukawa
kumuweka wazi mgombea wao wa urais huku kukiwa na eti eti huenda mmoja
wa vigogo wa CCM yuko mbioni kujiunga na umoja huo.
No comments:
Post a Comment