
Akiongea huko Seattle, USA walikopiga kambi kabla kuanza Mechi zao 4
za Ziara huko USA, Van Gaal alisema: "Hafuati falsafa yangu. Hamna
nafasi kwa Mtu kama hayo."
Valdes, Kipa wa Kimataifa wa Spain mwenye Miaka 33, hayumo kwenye Kikosi cha Wachezaji 27 ambao wako huko USA.
Valdes, aliewahi kutwaa Ubingwa wa La Liga mara 6 akiwa na
Barcelona, Mwaka Jana alijiunga na Man United na kufanya Mazoezi nao kwa
Miezi kadhaa baada ya Mkataba wake na Barca kumalizika wakati alipokuwa
akijiuguza Goti lake aliloumia vibaya na kisha kupewa Mkataba wa Miezi
18.
Akifafanua kutokuwepo Valdes huko Marekani, Van Gaal alisema:
"Mwaka Jana aligoma kuchezea Timu ya Pili na vipo vitu vingine
vinahitajika ukitaka kuwa Kipa wa United. Kama hufuati msimamo huo, ipo
njia moja tu na hiyo ni nje. Inasikitisha. Inahuzunisha kwa sababu
tulimpa nafasi apone na awe fiti, tukampa Mkataba na sasa yuko fiti
kucheza."
Valdes alicheza Mechi 3 za Timu ya Vijana ya U-21 Msimu uliopita
dhidi ya Liverpool, Chelsea na Tottenham kati ya Miezi Januari na Machi.
Mechi pekee ya Timu ya Kwanza aliyochezea ni ile ya mwisho kabisa
ya Msimu dhidi ya Hull City wakati Kipa Namba Moja David De Gea
alipoumia.
Kuhusu David De Gea anaehusishwa na kuhamia Real Madrid, Van Gaal
aliisema: "Siwezi kusema lolote. Yeye hana tatizo hapa. Ni ujinga
kuuliza."
Alipoulizwa kama Angel Di Maria atabaki Old Trafford huku kukiwa na
rippoti Mabingwa wa France Paris St-Germain wametoa Ofa kubwa kumnunua,
Van Gaal alijibu: "Sijui lolote. Tutaona. Kwa sasa bado ni Mchezaji wa
Manchester United."
No comments:
Post a Comment