Wednesday 12 August 2015

Wafanyakazi wanaojenga daraja la Kigamboni wagoma kushinikiza kuongezwa mshahara.


Ndoto za kukamilika kwa wakati kwa ujenzi wa daraja la Kigamboni zinazidi kufifia kutokana na wafanyakazi wanaojenga daraja hilo kuanza mgomo kushinikiza kuoingezwa mshahara huku wengine wakionyesha kuchoshwa na usumbufu wanaoupata na hivyo kudau kulipwa malimbikizi yao wakatafute kazi sehemu nyingine.
Hizo ni sauti za wafanyakazi hao wakiwa pembeni mwa daraja hilo wakishikiza kuongezwa fedha huku wakidaia kuwa kwa muda mrefu  wamefanyakazi kwa kunyonywa na sasa imefika mwisho.
 
Kufuatia hatua hiyo afisa kazi kutoka wizara ya kazi na ajira alifika katia eneo hilo na kuzungumza na wafanyakazi hao na kubainmisha mambo mbalimbali ya kisheria lakini wafanya kazi hao wakasisitza kulipwa kwanza haki zao kabla ya kuendelea na kazi.
 
Hata hivyo meneja mradi kutoka kampuni inayojenga daraja hilo kampuni ya REC mhandisi Liu Tao amesema wafanyakazi hao  walianza mgomo wa chini kwa chini tangu mwezi ulipotia na sasa wameamua kufanya mgomo wawazi wazi laki wameshandaa mpango wa kuwalipa fedha hizo.
 
Kwa upande wake meneja wa mradi upande wa barabara Bw Jamali Mruma amesema kwa kiasi kikubwa mgomo utahathiri ukamilikaji wa ujenzi wa daraja hilo ila jambo kubwa sasa ni kuona nini kifanyike ili kupunguza ukubwa wa tatizo.

No comments: