Friday 16 December 2016

C hama cha Waandishi wa Habari mkoani Mbeya kimetoa tamko la kupinga hukumu iliyotolewa dhidi ya dereva wa Shanta Mining alie sababisha ajali kwa waandishi watatu!!

Kulia ni mwenyekiti wa Chama Cha Waandishi wa Habari mkoa wa Mbeya Bw. Modest Nkulu akitoa taarifa kwa waandishi wa habari hawapo pichani, kushoto ni mweka hazina wa Chama cha Waandishi wa Habari mkoa wa Mbeya Bi. Esther Macha.
 

Waandishi wa Habari mkoani Mbeya wakimsikiliza kwa umakini Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari Bw. Modest Nkulu wakati akitoa tamko.
Wa kwanza kulia ni Bw. Gabriel Kandonga na wapili kutoka kulia ni Bi. Aines Thobias (wahanga wa ajali) wakisikiliza kwa umakini, wakati mwenyekiti Nkulu, wapili kutoka kushoto akitoa tamko la kupinga hukumu.

Chama cha waandishi wa habari mkoa wa Mbeya (MBPC) kimeeleza kuto kuwa na imani na hukumu iliyotolewa na Mahakama ya Wilaya ya Mbeya baada ya kumwachia huru Herman Joseph  mwenye (33) dereva  wa gari lenye  namba za usajiri T,321 CDA aina ya Toyota Land Cruiser mali ya Shanta Mining, ambaye aliwagonga waandishi  watatu ambao walikuwa wakitumia usafiri wa pikipiki aina ya King Loin yenye namba za usajili Mc 923 AZQ  uliyo kuwa ikiendeshwa na Gabriel Kandonga wakati wakitekeleza majukumu yao ya kikazi.

Akizungumza na waandishi wa habari wakati akitoa taarifa ya kuto ridhishwa na mwenendo wa kesi  pamoja na hukumu  Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Mbeya  (MBPC) ndugu Modestus Nkulu amesema ajali hiyo ambayo ilitokea mnamo tarehe 31/8/2016 katika barabara ya kutoka Mbalizi kuelekea Mkwajuni chunya ikihusisha gari aina ya Toyota Land Cruiser mali ya Shanta Maning  na  pikipiki ambayo ilikuwa ikitumiwa na waandishi wa habari ndugu Gabriel Kandonga, Ibrahim Yasin na Aines Thobias.

Mwenyekiti Nkulu amesema baada ya ajali hiyo, mnano tarehe 31.8.2016 kesi  yenye kumbukumbu namba MB/TR/RB/3828/2016 ilifunguliwa katika kituo cha mbalizi (Wilaya ya kipolisi Mbalizi) ambapo katika upelelezi ilishughulikiwa na WP 5830 CPL LUCY na mchoraji wa ramani ya ajali G 3944 PC MUSA wakati mkaguzi wa vyombo vya moto VIHECLE INSPECTOR wa polisi E 4677 CPL HAJI huku kesi iliyo sajiliwa kwa namba 108/2016 iliendeshwa na kusikilizwa chini ya Hakimu mkazi wa mahakama ya Wilaya Zawadi  Laizer na wakili wa serikali Catherin Paulokwa.

Aidha Nkulu akaeleza mazingira yaliyopelekea wanahabari mkoani Mbeya kukosa imani na mwenendo wa kesi pamoja  hukumu iliyotolewa mnano tarehe 13/12/2016 na mahakama hiyo ni kuendesha kesi bila mashahidi muhimu(wahanga wa tukio) kuitwa mahakamani, ambapo Nkulu alisema kufika kwa wahanga mahakamani kungesaidia mahakama kuona hali za majeruhi pamoja na uhalisia na ukubwa wa kosa.

Akifafanua zaidi mwenyekiti Nkulu amesema kuwa baada ya hukumu hiyo kutolewa uongozi wa chama cha waandishi wa habari wa mkoa wa mbeya ukiongozwa na Modest Nkulu ambae ni Mwenyekiti wa Mbeya Press Club  mnamo tarehe 14/12/2-16 ulilazimika kubisha hodi katika ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali ndugu Joseph Pande ili kuwasilisha masikitiko yao dhidi ya mwenendo wa kesi pamoja na hukumu iliyotolewa.

Aidha anaongeza kuwa baada ya kufanikiwa kufanya mazungumzo na mwanasheria mkuu wa mkoa wa mbeya ndugu Joseph Pande na kueleza masikitiko yake kuanzia mwenendo wa kesi tangu polisi, ofisi ya mwanasheria na mahakama, mwanasheria huyo alikiri ofisi yake kupokea taarifa ya upande wa mashitaka kushindwa hivyo ofisi yake imejipanga kushughulikia suala hilo kwa kukata rufaaa kupinga hukumu hiyo.

Hata hivyo katika kupinga hukumu hiyo chama cha waandishi wa habari mkoa wa Mbeya na wanachama wake walikuwa na tamko rasmi linalo ashiria kupiga hukumu hiyo likieleza maneno  yafuatayo  “Kwa umoja wetu kama waandishi wa habari mkoa wa Mbeya, tunapinga hukumu hiyo, kwa kuwa tunahisi haijazingatia haki na usawa kwa wahusika wote hususani wa jamhuri ambao ni walalamikaji”

No comments: