Saturday 17 December 2016

Gari la Mbunge Sugu lapata ajali na kuuwa mtoto.    

Gari la Mbunge wa Mbeya mjini Mh. Joseph Mbilinyi maarufu kwa jina la Sugu kupitia tiketi ya CHADEMA limepata ajali leo asubuhi ktk maeneo la iyunga na kusababisha kifo cha mtoto aliefahamika kwa jina moja la Rachael,

Wakati huo huo gari la trafiki ambalo lilikuwa likiwahi eneo la tukio ambalo  mbunge Joseph Mbilinyi amepatia ajali nalo likapata ajali katika maeneo ya Isanga ambapo trafiki wanne waliokuwepo katika gari hilo wamenusurika kifo, kati yao watatu wa walipata matibabu katika Hospital ya Rufaa Mbeya na kuruhusiwa na mmoja ambae alipata jeraha kichwani anaendelea kupata matibabu ambapo kwa mujibu wa muuguzi msaidizi wa zamu hospital ya rufaa Mbeya  bw. Hamisi Myongo amesema askari huyo ataruhusiwa leo hii baada ya  matibabu kukamilika. 
Kwa upande wake mbunge Sugu ambae hakuwa tayari kuzungumzia zaidi ajali hiyo amesema wakati ajali hiyo ikitokea nae alikuwa ktk gari hilo ambalo lilikuwa likiendeshwa na dereva wake  ambapo amesema amesikitishwa na tukio hilo 

Na Asha Athuman

No comments: