Waziri
Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa amepokea
msaada wa magari matatu yenye thamani ya Dola za Marekani 99,700 kutoka
Kampuni ya Foton International Trade Co. Ltd ya nchini China.
Majaliwa
amepokea msaada huo jana Agosti 9, 2017 jijini Dar es Salaam, ambapo
alisema magari hayo yatatumika katika shughuli mbalimbali za maendeleo
ya jamii nchini. Magari hayo ni Sauvana SUV moja na Tunland Double cabin
mbili.
“Nashukuru
kwa msaada huu wa magari uliotolewa na Kampuni ya Foton kwa Serikali
yetu. Magari haya yanaweza kutumika katika Hospitali za wilaya kwa ajili
ya usambazaji wa dawa na vifaa tiba pamoja na kutolea elimu mbalimbali
kwa umma.”
Naye,
Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo Zhao Xiao alisema wametoa
msaada huo wa magari kwa ajili ya kusaidia shughuli za maendeleo
zinazofanywa na Serikali ya Tanzania hususan maeneo ya vijijini.
Xiao
alisema Kampuni ya Foton inatengeneza magari 700,000 kwa mwaka, ambayo
yanauzwa katika nchi 125 duniani. Amesea ifikapo mwaka 2020 wanatarajia
kuongeza uzalishaji na kufikia magari milioni 1.4 kwa mwaka.
Kuhusu
suala la kuja kuwekeza kwenye ujenzi wa kiwanda cha kuunganisha magari
nchini, Bw. Xiao alisema wanampango wa kuwekeza nchini kwa kuwa kuna
fursa nzuri za uwekezaji na uhakika wa masoko katika nchi zingine za
Afrika Mashariki.
No comments:
Post a Comment