Tuesday 5 September 2017

Mwijage Kutua India Kuisafisha Tanzania


SeeBait
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Charles John Mwijage  amekiri kupokea wito wa kwenda nchini India kwa ajili ya kusafisha jina la Tanzani baada ya watu wanaodaiwa ni madalali tapeli wa zao korosho kulichafua.

Mh. Mwijage ameyasema hayo jana ambapo amedai kuwa anaoushahidi  kuwa kampuni hizo za udalali zilichafua jina la nchi hivyo ni lazima awafikishe katika mikono yua sheria.

“Vitendo hivi vinavyofanywa na makampuni haya havivumiliki kwani mchezo huu ni mauti kwetu na nitahakikisha wanachukuliwa hatua kwani ninao ushahidi unaotosheleza,”alisema Mwijage.

Mh. Mwijage amefafanua kwa kusema kwamba watu wametapeliwa kwa kuambiwa pindi wanapoagiza mazao watoe pesa ya kianzio ambayo ni kuanzia dola za Marekani 123,000, sawa na Sh275 milioni na dola 200,000 sawa na Sh448milioni za kitanzania.

“Nimepokea wito kutoka India kwa ajili ya kwenda kusafisha jina la nchi kutokana na taswira iliyosababishwa na uwepo wa matapeli hao,”alisema Mwijage.

No comments: