Katibu
Mkuu wa Chadema, Dk Vincent Mashinji ametakiwa kuripoti ofisi ya
Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), imeelezwa.
Dk
Mashinji anakwenda kuripoti kipindi ambacho Mkurugenzi wa Operesheni na
Mafunzo wa chama hicho, Kigaila Benson anaendelea kushikiliwa katika
Kituo Kikuu cha Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam.
Mwanasheria
wa Chadema, Fredrick Kihwelo amesema, “Katibu Mkuu ametakiwa kuripoti
kwa DCI na sasa natoka hapa Central kwa Kigaila nakwenda huko."
Amesema
suala la Kigaila kupata dhamana au kupelekwa mahakamani litajulikana
mchana wa leo baada ya kutakiwa kurudi Kituo Kikuu cha Polisi.
Kihwelo
alipoulizwa ni nini sababu ya Dk Mashinji kuitwa kwa DCI, amesema
itakuwa ni mwendelezo wa mahojiano na Jeshi la Polisi kuhusu tuhuma za
kutoa lugha za uchochezi alipozungumzia hali ya afya ya Mbunge wa
Singida Mashariki, Tundu Lissu.
Kigaila
ambaye ameshafikisha saa 72 akiwa rumande tangu alipojisalimisha
kituoni hapo Jumatatu Oktoba 23,2017 na kuhojiwa kwa kutoa lugha za
uchochezi katika mkutano na wanahabari Oktoba 12,2017 makao makuu ya
Chadema wilayani Kinondoni mkoani Dar es Salaam.
No comments:
Post a Comment