Mbunge
wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari ametoa onyo kwa viongozi wa
Serikali ya Arusha, akiwepo Mkuu wa Mkoa pamoja na Mkuu wa Wilaya ya
Arumeru kwamba waache kuwatishia wagombea wa chama chake (CHADEMA)
ikiwepo kuwashawishi waajiondoe kwenye uchaguzi wa madiwani unaotarajiwa
kufanyika Oktoba 26.
Mh.
Nassari amewaonya viongozi hao huku akiwakumbusha kwamba wanatakiwa
wafahamu wana-deal na watu wa aina gani huku akiwakumbusha kwamba kama
wanataka kurekodiwa.
"Onyo
kwa RC na DC! acheni kuwatisha wagombea wetu, acheni kuwatuma watu
wakiwemo viongozi wa dini kuwashawishi wajiondoe kwa ahadi zilezile.
Mmesahau mna-deal na watu wa aina gani?? Au bado mnataka kurekodiwa??"
Ameandika Nassari katika mtandao wake wa Facebook.
Ameongeza kwamba "We are determined, (Tumedhamiria) Tukutane kwa debe!!"
Mapema
mwezi huu Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) ilitangaza kwamba uchaguzi
mdogo wa marudio wa madiwani katika kata 43 utafanyika Novemba 26 mwaka
huu, huku Arusha ikiwa imepoteza kata kumi.
No comments:
Post a Comment