Kiongozi wa Jumuiya ya Ismailia, Mtukufu Aga Khan amesema wamedhamiria kuunga mkono juhudi za Serikali kwa kupanua hospitali.
Amesema
Hospitali ya Aga Khan jijini Dar es Salaam itapanuliwa na pia watajenga
chuo kikuu kikubwa katika ukanda wa Afrika Mashariki mkoani Arusha.
Mtukufu Aga Khan amesema hayo jana Jumatano Ikulu jijini Dar es Salaam, alipofanya mazungumzo na Rais John Magufuli.
Alisema
upanuzi wa hospitali utahusisha kuongeza idadi ya vitanda vya wagonjwa
kutoka 72 vya sasa hadi 172, kuimarisha matibabu ya moyo na saratani.
Taarifa
ya Ikulu kwa vyombo vya habari imesema upanuzi wa hospitali pia
utahusisha ufundishaji wa madaktari na wataalamu wengine wa afya.
Kuhusu
chuo kikuu, Mtukufu Aga Khan alisema jumuiya imedhamiria kujenga
kikubwa ambacho kitafundisha viongozi si tu wa Tanzania na Afrika
Mashariki, bali Afrika nzima ili wawe chachu ya mabadiliko na maendeleo.
Rais John Magufuli katika taarifa hiyo alimshukuru Mtukufu Aga Khan kwa taasisi zake kutoa huduma za kijamii nchini Tanzania.
Alitoa
wito kwa taasisi hizo kupunguza gharama za huduma ili wananchi wamudu
na hasa ikizingatiwa kuwa zimekuwa zikipata msamaha wa kodi kutoka
serikalini.
Rais
Magufuli alisema Serikali ipo tayari kuendeleza na kuimarisha
ushirikiano na Aga Khan na amemuomba kiongozi huyo wa dini kuendelea
kupanua wigo wa huduma za taasisi zake ikiwa ni pamoja na kuwekeza mjini
Dodoma yaliko makao makuu ya Serikali.
No comments:
Post a Comment