Monday 20 April 2015

MTABIRI AMPA JIDE UHAKIKA WA KUZAA

Staa wa Bongo Fleva, Judith Wambura 'Jide' na Mtabiri maarufu Bongo, Maalim Hassan Yahaya Hussein.
Staa wa Bongo Fleva, Judith Wambura 'Jide'.
Mtabiri maarufu Bongo, Maalim Hassan Yahaya Hussein.
Gladness Mallya na Gabriel Ng'osha
Habari njema! Kufuatia wimbi la baadhi ya mastaa kulia na tatizo la ugumba, mtabiri maarufu Bongo, Maalim Hassan Yahaya Hussein, amemtabiria mema staa wa Bongo Fleva, Judith Wambura 'Jide' kwamba endapo atatafuata tiba mbadala, atapata mtoto mwaka huu.
Akizungumza na Ijumaa Wikienda, Maalim Hassan alisema kwamba, huu ni mwaka wa mafanikio kwa Jide ambayo mwenyewe yatamshangaza likiwemo suala la mtoto kama atachukua hatua ya kuwaona wataalam wa tatizo lake ambalo aliwahi kulitoa kwenye kipindi chake cha Diary ya Lady Jaydee kupitia EATV la jini mahaba.
Alieleza kwamba jini mahaba huwa lina madhara makubwa kwa mwanamke na ndilo linalowasumbua wengi kwani wanapima vipimo vyote hospitali na kuonekana wana uwezo wa kuzaa lakini wanashindwa kutokana na tatizo hilo.
"Jide aje kwangu nitamsaidia na ndani ya mwaka huu atapata mtoto maana nyota yake inaonyesha mafanikio mengi au kama akishindwa kuja kwangu basi atafute wataalam wa mambo ya majini, watamsaidia kwani hana tatizo la ugumba ila kukosa kwake mtoto kunatokana na jini mahaba ambalo likimshika mwanamke anajikuta akikosa mtoto," alisema Maalim Hassan.
Aliongeza kwamba wasanii wengi wa kike wamekuwa wakilalamikia suala la kukosa watoto japokuwa wengine wana tatizo hilo la jini mahaba huku wengine wakitoa mimba na inapofika wakati wa kutaka watoto, wanakosa kwani mayai yanakuwa yameisha.

No comments: