Sunday 6 March 2016

Breaking News : Rais Magufuli Amteua Balozi John Wiliam Kijazi Kuwa Katibu Mkuu Kiongozi.......Ombeni Sefue Atapangiwa Kazi Nyingine

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli amemteua Balozi Mhandisi John William Kijazi kuwa Katibu Mkuu Kiongozi. 

Kabla ya uteuzi huo Mhandisi Kijazi alikuwa Balozi wa Tanzania nchini India.

Kufuatia uteuzi huo, aliyekuwa Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue atapangiwa kazi nyingine.

Gerson Msigwa

Kaimu Mkurugenzi  wa Mawasiliano, IKULU

Dar es Salaam

06March,2016


No comments: